Connect with us

News

Rais Ruto atia saini Miswada miwili kupiga jeki Mgao wa Serikali za Kaunti

Published

on

Rais William Ruto ametia saini na kuwa sheria miswaada miwili muhimu inayokusudiwa kupiga jeki ufadhili wa Serikali za Ugatuzi nchini.
Rais Ruto ambaye anahudhuria Kongamano la Ugatuzi mwaka huu katika kaunti ya Homa Bay, ametia saini mswada kuhusu Ugavi wa pato la serikali kwa hazina za Kaunti wa 2025, na pia Mswada mwengine unaotoa muongozo wa matumizi ya fedha za serikali za Kaunti wa 2023.
Mswaada unaohusu usimamizi na muongozo wa matumizi ya pesa za kaunti sasa umefutiliwa mbali na kubuni Hazina ya mabunge ya Kaunti zote 47.
Mswaada huo wa nyongeza ya pato kwa kaunti umeongoza kiwango cha hapo awali kutoka Shilingi billioni 387.4 mwaka uliopita hadi kiwango cha Shilingi bilioni 415 katika kipindi cha mwaka huu 2025/26 cha matumizi ya pesa serikalini.
Hafla hiyo ya kutia saini miswaada hiyo miwili,imefanyika katika Ikulu ndogo kaunti ya Homabay Jumatano Agostu 13 2025.
Mswaada huo uliowasilishwa bungeni na Senta wa Meru Kathuri Murungi, unayapa uhuru zaidi Mabunge ya Kaunti katika masuala ya usimamizi wa fedha zao.

Hatua hiyo imetokea wakati Kongamano la Ugatuzi limefunguliwa rasmi katika Kaunti ya Homabay, kutathmini mafanikio na changamoto kwa serikali za Kaunti.
Kongamano hilo linahudhuriwa miongoni mwa wengine Wafanyi biashara na washika Dau mbali mbali wa kimaendeleo katika ngazi za Kaunti.
Hazina kuu ya Serikali sasa inatarajiwa kuhakikisha kuwa mgao huo wa fedha unafikia hazina za serikali za Kuanti kabla ya tarehe 15 ya kila mwezi

Katika muda wa miaka miwili iliyopita serikali kuu ya kitaifa imeshtumiwa vikali na Baraza la Magavana, kwa madai ya njama za kuhujumu Ugatuzi nchini.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Waziri wa zamani Dalmas Otieno Afariki

Published

on

By

Mbunge wa zamani wa eneo bunge la Rongo Dalmas Otieno ameaga dunia.

Kiongozi huyo shupavu na mweledi katika uzungumzaji, ameaga dunia Septemba 7, 2025 nyumbani kwake katika mtaa wa Kileleshwa jijini Nairobi.

Marehemu ambaye aliwahi shikilia Wizara mbalimbali nchini pamoja na taasisi za umma muhimu kuanzia utawala wa Rais wa pili nchini Hayati Daniel Arap Moi katika miaka ya 80 atakumbukwa na wengi kwa mchango wake nchini.

Taarifa za Kifo chake zimetolewa na mwanawe Eddy Otieno.

Otieno alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuingia bungeni na kuwaakilisha eneo bunge la Rongo mnamo mwaka 1988, na kisha baadaye kuhudumu kama Waziri wa ustawi wa viwanda kati ya 1988-1991.

Mwaka wa 1991 aliteuliwa kuwa Waziri wa Leba, lakini pia akahudumu kama Waziri uchukuzi na mawasiliano chini ya utawala wa Rais Daniel Toroitich Arap Moi.

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula wametaka Mwendazake kama kiongozi alichagia mengi nchini hasa suala zima la maendeleo na miswada muhimu bungeni.

Mungu ailaze roho yake pema Peponi.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

News

Baraza la vyombo vya habari MCK lakerwa na baadhi ya vyombo habari

Published

on

By

Baraza la vyombo vya habari nchini MCK limeeleza kusikitishwa na hatua ya baadhi ya vyombo vya habari nchini kumwingilia rais wa chama cha mawakili LSK Faith Odhiambo baada ya kukubali kujumuishwa kwenye kamati ya kuangazia fidia kwa waathiriwa wa maandamano nchini.

MCK ilisema hatua ya Odhiambo kujumuishwa katika kamati hiyo kuhakikisha waathiriwa wa maandamano hayo wanapata haki kwa mujibu wa sheria.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, baraza hilo lilipongeza juhudi za vyombo vya habari kwa kuangazia kwa undani maandamano yaliyofanyika nchini na hata baadhi ya wanabari kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani.

MCK ilisema hatua ya baadhi vyombo vya habari kukosoa mwelekeo wa Odhiambo kunaiweka LSK katika hatari ya ukosoaji zaidi, katika juhudi za kuangazia usawa kwenye maswala ya uongozi dhabiti nchini.

Taarifa ya baraza la vyombo vya habari nchini MCK.

Ilieshinikiza wakenya kufahamu kuwa chama cha LSK kinaongozwa na taasisi muhimu za umma ikiwepo idara ya mahakama, ofisi ya mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma, ofisi ya mkuu wa sheria nchini vile vile tume ya malalamishi kwa vyombo vya habari.

MCK ilivitaka vyombo vya habari kumruhusu Odhiambo kuendelea kutekeleza majukumu yake bila muingilio katika kamati hiyo.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending