Connect with us

News

Bi Rachel azindua mpango wa “lishe bora” shuleni

Published

on

Ofisi ya mke wa Rais Bi Rachel Ruto, imezindua mpango wa lishe bora kupitia utoaji wa maziwa kwa watoto wa shule kama sehemu ya mpango wa kuboresha afya na kuongeza nguvu kwa watoto ili waweze kuendelea na masomo yao shuleni bila changamoto zozote.

Akingumza katika Shule ya msingi ya Kachororoni eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Bi Rachel alisema mpango huo wa Feed One End Hunger ambao umefanikishwa kwa ushirikiano na Bodi ya Maziwa nchini KDB na Muungano wa ushirika wa maziwa, Meru utadhibiti utapiamlo kwa watoto.

Bi Rachel Ruto alisema wanafunzi wengi nchini ambao wanatoka kwenye familia zisizojiweza hasa kifedha wamekuwa wakisitisha masomo yao kutokana na njaa na utapiamlo kutokana na ukosefu wa lishe bora.

“Afya ya mtoto ni muhimu sana na ikiwa mpango huu wa lishe bora utakumbatiwa, wanafunzi wengi shuleni watafanya vyema katika masomo yao”, alisema Bi Rachel Ruto.

Kwa upande wake Katibu mkuu katika Wizara ya Kilimo nchini Jonathan Mueke ambaye alikuwa ameandamana na Bi Rachel Ruto aliupongeza mpango huo akiutaja kama hatua muhimu ya kufanikisha elimu shuleni.

Naye Naibu Gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule alisema tangu kuzinduliwa kwa mpango wa lishe shuleni kaunti ya Kilifi, wanafunzi wengi wamekuwa wakijiunga na shule mbalimbali ikilinganishwa na miaka ya nyuma na kuahidi kushirikiana na ofisi ya mke wa rais Bi Rachel Ruto katika kuhakikisha unafikishwa vilivyo.

Hata hivyo Mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu Tungule alitoa wito kwa Rais William Samoei Ruto kujenga barabara ya Kilifi – Ganze – Bamba ili kuimarisha shughuli za uchukuzi eneo hilo.

Kauli ambayo iliungwa mkono na Mwakilishi wa Kike kaunti ya Kilifi Getrude Mbeyu, ambaye alisema eneo bunge la Ganze lina raslimali nyingi na huenda Ganze ikawa eneo tajiri zaidi nchini iwapo raslimali hizo zitatumika ipasavyo na kuipongeza Serikali kuu kupitia Wizara ya Utalii na wanyamapori nchini kutoa kima cha shilingi milioni 60 za fidia kwa wakaazi wa kaunti ya Kilifi walioathiriwa na wanyamapori.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending