Connect with us

News

Polisi wasimamishwa kazi kwa kumpiga risasi mchuuzi.

Published

on

Huduma ya kitaifa ya polisi NPS imewasimamisha kazi maafisa wawili wa polisi wanaohusishwa na kisa cha kupigwa risasi raia ambaye hakuwa na silaha wakati maandamano ya kushinikiza naibu inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu siku ya jumanne 17, Juni 2025 jijini Nairobi.

Maafisa hao wawili hao, Konstebo Klinzy Barasa Masinde na Duncan Kiprono, walinaswa katika video ambayo sasa inasambaa mitandaoni ikionyesha afisa mmoja akimpiga risasi mchuuzi wa barakoa, na kumwacha akidhania kuwa amefariki kwenye barabara ya Moi Avenue jijini Nairobi.

“Maafisa hao wawili sasa wamesimamishwa kazi na wanashughulikiwa na kitengo cha maafisa wa kukabiliana na mauaji, makao makuu ya maafisa wa upelelezi wa makosa ya jinai-DCI, wakisubiri hatua zaidi,” ilisoma taarifa hiyo iliyotiwa saini na msemaji wa NPS Muchiri Nyaga.

Huduma ya polisi iliongeza kuwa mwanamme aliyejeruhiwa, hali yake ya afya inaendelea vyema katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta jijini Nairobi baada ya kufanyiwa upasuaji.

“Huduma ya kitaifa ya polisi NPS inajutia sana kitendo hiki kisicho na msingi na inamuhurumia mwathiriwa na familia yake, huku ikisisitiza kujitolea kwake kikamilifu kuhakikisha haki inatendeka,” iliongeza taarifa hiyo.

Hatua ya kuwatambua maafisa hao ilitokana na lalama za wananchi kushinikiza  huduma ya polisi nchini kubaini waliohusika katika kosa hilo.

Maandamano hayo yaliyomtaka naibu inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat ajiuzulu, yaligeuka na kuwa machafuko baada ya wahuni kuingilia kati na kutatiza waandamanaji.

Katika mojawapo ya video ambazo zilizua taharuki kwa umma, maafisa hao walimkabili mchuuzi huyo wa barakoa ambaye hakuwa na silaha kabla ya mmoja wao kufyatua risasi akiwa karibu.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending