News
Polisi wasimamishwa kazi kwa kumpiga risasi mchuuzi.

Huduma ya kitaifa ya polisi NPS imewasimamisha kazi maafisa wawili wa polisi wanaohusishwa na kisa cha kupigwa risasi raia ambaye hakuwa na silaha wakati maandamano ya kushinikiza naibu inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu siku ya jumanne 17, Juni 2025 jijini Nairobi.
Maafisa hao wawili hao, Konstebo Klinzy Barasa Masinde na Duncan Kiprono, walinaswa katika video ambayo sasa inasambaa mitandaoni ikionyesha afisa mmoja akimpiga risasi mchuuzi wa barakoa, na kumwacha akidhania kuwa amefariki kwenye barabara ya Moi Avenue jijini Nairobi.
“Maafisa hao wawili sasa wamesimamishwa kazi na wanashughulikiwa na kitengo cha maafisa wa kukabiliana na mauaji, makao makuu ya maafisa wa upelelezi wa makosa ya jinai-DCI, wakisubiri hatua zaidi,” ilisoma taarifa hiyo iliyotiwa saini na msemaji wa NPS Muchiri Nyaga.
Huduma ya polisi iliongeza kuwa mwanamme aliyejeruhiwa, hali yake ya afya inaendelea vyema katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta jijini Nairobi baada ya kufanyiwa upasuaji.
“Huduma ya kitaifa ya polisi NPS inajutia sana kitendo hiki kisicho na msingi na inamuhurumia mwathiriwa na familia yake, huku ikisisitiza kujitolea kwake kikamilifu kuhakikisha haki inatendeka,” iliongeza taarifa hiyo.
Hatua ya kuwatambua maafisa hao ilitokana na lalama za wananchi kushinikiza huduma ya polisi nchini kubaini waliohusika katika kosa hilo.
Maandamano hayo yaliyomtaka naibu inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat ajiuzulu, yaligeuka na kuwa machafuko baada ya wahuni kuingilia kati na kutatiza waandamanaji.
Katika mojawapo ya video ambazo zilizua taharuki kwa umma, maafisa hao walimkabili mchuuzi huyo wa barakoa ambaye hakuwa na silaha kabla ya mmoja wao kufyatua risasi akiwa karibu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu