Connect with us

News

Polisi wamewakamata washukiwa 6 wa uhalifu, Mombasa

Published

on

Maafisa wa Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI kaunti ya Mombasa wamewakamata washukiwa 6 wa uhalifu wa mtandao wanaoshukiwa kuhusika na ulaghai kwa kutumia teknolojia ya kubadilisha namba za simu (caller ID spoofing), kwa lengo la kuwahadaa wananchi na kuwaibia pesa.

Washukiwa hao ni pamoja na Fortune Muthina Kinyanzui almaarufu Albanas Kyalo, Ruel Kipkoech Yator almaarufu Papa Ruel, Laban Kipkirui Koech, Weldon Kipyegon Rono, Towet Kipkorir Alphonce na Kelvin Kipyegon Koech.

Washukiwa hao wanadaiwa kuwapigia simu waathiriwa wakijifanya kuwa wahudumu wa wateja wa benki au kampuni za simu na kisha kuwahadaa watoe taarifa zao kama namba za vitambulisho, nambari za siri (PIN) na taarifa nyingine muhimu za kifedha ambazo walizitumia kuiba pesa kutoka kwa akaunti zao.

Inadaiwa kuwa Fortune Muthina, ambaye ni kiongozi wa genge hilo ndiye anayemiliki mfumo huo wa kudanganya namba za simu, ambayo alikuwa anakodishia matapeli wengine kuitumia kwa ada ya zaidi ya shilingi laki tano.

Washukiwa hao walikamatwa katika nyumba waliokuwa wamekodi na kujificha ili kutekeleza uhalifu huo ambapo maafisa wa polisi walifanikiwa kupata simu 19, laini za simu kutoka mitandao tofauti ya mawasiliano pamoja na daftari lenye majina na taarifa za watu wanaoshukiwa kuwa waathiriwa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Gachagua, amkosoa Rais Ruto kwa madai ya uongozi duni

Published

on

By

Viongozi wa upinzani nchini wakiongozwa na Kinara wa Chama cha Wiper Kalonzo Musyoka na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua waliendeleza kampeni za Wantam dhidi ya rais William Ruto wakielenga uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.

Wakazingumza wakati wa ziara yao ya kisiasa katika eneo la Pwani, Kalonzo alimkosoa rais Ruto akisema ameshindwa kuongoza taifa hali na kuendelea kuwanyanyasa vijana wa Gen Z kwa kuwateka nyara kiholela.

Kalonzo hata hivyo alidai kwamba serikali ya Kenya kwanza ina malengo fiche dhidi ya Bandari ya Mombasa, akisema kama wapinzani watahakikisha serikali ya rais Ruto ina hudumu kwa muhula moja pekee.

“Rais Ruto alishindwa kuongoza nchi na kuendelea kuwanyanyasa wakenya hasa vijana wa Gen Z kwani tumeshuhudia utekaji nyara wa kiholela na hata bandari ya Mombasa wako na malengo fiche na hiyo”, alisema Kalonzo.

Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na ambaye pia ni Kinara wa Chama cha DCP, amemkosoa rais Ruto na Katibu wa Muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli kwa kuwahadawa wakenya na kusambaratisha uchumi wa nchi pamoja na kufuja fedha za hazina ya NSSF huku Atwoli akilinyamazia suala hilo.

“Pesa ya NSSF imechukuliwa na Rais Ruto na kuendelea kujenga barabara na Bomas hiyo ni kinyume na sheria na hatutakubali na yule kiongozi wa kutetea wafanyikazi Atwoli amenyamaza ama wamekula hiyo pesa pamoja”, alisema Gachagua.

Upinzani waendeleza kampeni za Wantam

Hata hivyo viongozi walioandamana na Kalonzo katika ziara hiyo ya kisiasa eneo la Pwani wakiongozwa na Mgombea wa kiti cha ubunge wa eneo bunge la Magarini Furaha Chengo Ngumbao, walisema serikali imesheheni wizi wa mashamba ya wakaazi wa Pwani na kudia kwamba mamlaka yote yako nchini ya wananchi.

Wengine walioandamana na Kalonzo ni pamoja na Naibu Kinara wa DCP Cleophas Malala, Mbunge wa Wundanyi Danson Mwashako, Seneta wa Kisii Richard Onyonka miongoni mwa viongozi wengine.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending