Connect with us

Sports

Police Bullets Kuanza kampeni ya CECAFA kwa matarajio ya kutwaa ubingwa

Published

on

Mkufunzi wa kilabu ya Kenya Police Bullets, Beldine Odemba, amesema timu yake iko tayari kupambana hadi mwisho na kutwaa ubingwa wa CECAFA Qualifiers za Ligi ya Mabingwa wa Wanawake wa CAF.

Mabingwa wa FKF Women’s Premier League wataanza kampeni yao siku ya hapo kesho, Septemba 4, 2025, dhidi ya Kampala Queens ya Uganda katika Uwanja wa Nyayo National Stadium. Wapo Kundi A, ambalo pia linajumuisha Denden FC ya Eritrea.

Kundi B lina mabingwa watetezi Commercial Bank of Ethiopia (CBE), pamoja na Top Girls Academy ya Burundi na Rayon Sports WFC ya Rwanda.
Kundi C linaongozwa na JKT Queens ya Tanzania, wakijiunga na Yei Joint Stars ya Sudan Kusini na JKU Princess ya Zanzibar.

“Wasichana wako tayari kabisa kuanza mashindano ya CECAFA.wamepata mafunzo makali na naamini faida ya kucheza nyumbani itatufanikisha kutwaa taji na kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa wa Wanawake wa CAF. Kama nilivyosema awali, tutaheshimu kila timu na hatuwezi kuidharau timu yoyote,” alisema Odemba.

Mwalimu huyo akiwahimiza mashabiki kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nyayo Stadium na Ulinzi Complex kuwashangilia Bullets.

Kwa Police Bullets, dhamira ni ya kulipiza kisasi.

Mwaka jana mjini Addis Ababa, walikaribia kufuzu lakini wakapoteza 1-0 dhidi ya CBE kwenye fainali. Safari hii, wamedhamiria kutumia nafasi yao ipasavyo wakiwa nyumbani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Sinner na Alcaraz Wakutana Tena Fainali ya US Open Baada ya Muitaliano Kufuzu Fainali ya Tano Mfululizo ya Grand Slam

Published

on

By

Bingwa taji la US Open mchezo wa tenisi Jannik Sinner anatarajia mechi ya kipekee na “maalum” atakapokutana na mchezaji wa pili duniani Carlos Alcaraz raia wa Uhispania kwenye fainali ya wanaume ya US Open baada ya Muitaliano huyo kufuzu kwa fainali yake ya tano mfululizo ya Grand Slam siku ya Ijumaa.

Sinner alimshinda Felix Auger-Aliassime kwa seti 6-1, 3-6, 6-3, 6-4 na sasa analenga taji lake la tano la Grand Slam baada ya kujiunga na Rod Laver, Roger Federer na Novak Djokovic kama wanaume pekee kufika fainali zote nne za Grand Slam katika msimu mmoja.

“Nadhani kufika fainali tano mfululizo za Grand Slam ni jambo kubwa. Uthabiti na kujiweka katika hatua za mwisho za mashindano makubwa tuliyonayo, ni kitu cha kushangaza,” alisema Sinner.

Nafasi yake ya kwanza duniani itakuwa hatarini Jumapili wakati atakapokutana na Alcaraz kwa mara ya tatu mfululizo katika fainali ya Grand Slam.

Sinner mwenye umri wa miaka 24 alitwaa mataji ya Australian Open na Wimbledon msimu huu lakini alifungwa na Alcaraz mwenye miaka 22 katika pambano kali la seti tano kwenye French Open.

“Uwanjani tunapenda kukutana, unajua, kwa sababu kutokana na nafasi zetu kwenye viwango, inamaanisha tunafanya vizuri kwenye mashindano,” alisema Sinner.

Watakutana tena US Open kwa mara ya pili. Mchuano wao wa kwanza ulikuwa robo-fainali ya 2022, pambano kubwa lililounda ushindani wao.

“Jumapili ni siku maalum sana na fainali ya kushangaza tena,” alisema Sinner. “Ninahisi ushindani wetu ulianza hapa kwa kucheza mechi ya ajabu. Sasa sisi ni wachezaji tofauti, wenye kujiamini zaidi pia.”

Miaka mitatu iliyopita, Alcaraz ndiye aliyeshinda baada ya pambano lililodumu saa 5 na dakika 15 na kumalizika kabla ya saa 9 alfajiri huko New York, na Mspaniola huyo akaenda kunyanyua taji lake la kwanza la Grand Slam kwenye mashindano hayo.

Sinner analenga kumshinda Alcaraz Jumapili kwa kutwaa taji lake la tano la Grand Slam. Mafanikio hayo yamejengwa zaidi kwenye ushindi wa mechi 27 mfululizo za Grand Slam kwenye uwanja wa hard court.

Analenga kuwa mwanaume wa kwanza kutetea taji la US Open tangu Federer alipochukua la mwisho kati ya mataji yake matano mfululizo mwaka 2008.

Mkanada Auger-Aliassime alikuwa akijaribu kufuzu kwa fainali yake ya kwanza ya Grand Slam baada ya kufika nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu safari yake hadi hatua hiyo hiyo kwenye US Open mwaka 2021.

“Sina majuto. Nilicheza kwa njia yangu. Nilicheza mchezo wangu. Unajua, kwa namna fulani unaishi na kufa na maamuzi yako,” alisema Auger-Aliassime.

Continue Reading

Sports

Ndoto ya Harambee Stars ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 Yagonga mwamba baada ya kupigwa 3-1 na Gambia Kasarani

Published

on

By

Ndoto ya Harambee Stars ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la FIFA 2026 ilizimwa rasmi hapo jana baada ya kuchapwa mabao 3-1 na The Scorpions ya Gambia katika mechi ya kufuzu ya Kundi F la CAF iliyochezewa Uwanja wa Kasarani.

Scorpions, wakiongozwa na kocha wa zamani wa Gor Mahia Jonathan McKinstry, walitoa mchezo wa kiukatili katika kipindi cha kwanza dhidi ya vijana wa Benni McCarthy, na kuhuisha matumaini yao ya kufuzu kwa fainali zitakazofanyika Marekani, Kanada na Mexico.

Harambee Stars, waliokuwa na matumaini finyu ya kufuzu, walizidiwa maarifa na upande wa Gambia uliokuwa makini zaidi, uliodhibiti mchezo ndani ya dakika 30 za kwanza.

Udhaifu wa safu ya ulinzi ya Kenya ulionekana mapema dakika ya 12 pale Sulayman Sinyan alipofunga kwa kichwa akimalizia kona ya ndani ya Yankuba Minteh, mshambuliaji wa Brighton & Hove Albion, na kuwaweka Stars kwenye presha.

Minteh, aliyewasumbua mabeki wa Kenya mara kwa mara, aliongeza bao la pili dakika ya 26 kwa shuti la utulivu lililokwenda chini kushoto baada ya kuchukua faida ya makosa ya safu ya kiungo ya Kenya.

Gambia waliongeza bao la tatu dakika ya 38 kupitia Musa Barrow aliyepiga shuti kali la volley lililoenda moja kwa moja hadi kona ya mbali ya goli, na kufunga rasmi mchezo.

Safu ya ulinzi ya Kenya iliendelea kuonekana dhaifu, na hasira zikadhihirika katika muda wa nyongeza wa kipindi cha kwanza pale Collins Sichenje alipokumbwa na kadi ya njano kufuatia rafu mbaya – hali iliyomwacha kocha McCarthy akiwa mwenye hasira pembeni mwa uwanja.

Stars walionekana kufufuka baada ya mapumziko kufuatia mabadiliko mawili ya wachezaji yaliyoongeza nguvu, na juhudi zao ziliwalipa dakika ya 81.

Ryan Ogam, aliyeingia kutoka benchi, alipiga shuti kwa mguu wake dhaifu wa kulia katikati ya kisanduku na kufunga bao lililoleta matumaini kwa wenyeji.

Hata hivyo, ilikuwa ni kuchelewa mno kwani wageni waliweza kudhibiti mchezo hadi mwisho na kuondoka na alama zote tatu.

Matokeo hayo yanaiweka Kenya ikiwa na pointi 6 pekee katika Kundi F, na ndoto yao ya Kombe la Dunia 2026 ikizimika rasmi licha ya kubakisha mechi tatu.

Kwa upande wa Gambia, ushindi huu uliwapandisha juu ya Kenya na kuweka hai matumaini yao ya kufuzu, ingawa wanakabiliwa na changamoto kubwa dhidi ya Burundi na Gabon.

Kwa Kenya, macho sasa yanaelekezwa kwenye mchezo wa nyumbani dhidi ya UShelisheli siku ya Jumanne ambapo watatumai kumaliza mapumziko ya kimataifa kwa ushindi, huku wakiangazia maandalizi ya kampeni ya AFCON 2027.

Continue Reading

Trending