Connect with us

News

Pigo kwa Spika Mwambire, apokonywa walinzi

Published

on

Karani wa bunge la kaunti ya Kilifi Emmanuel Ngala ameagiza kuondolewa kwa walinzi wanaolinda makaazi ya Spika wa bunge la kaunti hiyo Teddy Mwambire.

Kulingana na barua iliyoandikwa na Ngala kupitia bunge hilo na kuwasilishwa kwa Spika Mwambire, walinzi wote ambao wanalinda makaazi ya Spika huyo kupitia kampuni ya Ulinzi ya Ismax, hawatatekeleza tena majukumu yao.

Barua hiyo pia imefafanua kwamba hatua hiyo ni kutokana na bunge la kaunti ya Kilifi kumtimua Mamlakani Spika Mwambire Juni 30 mwaka huu baada ya Wawakilishi wadi 40 kati ya 51 kupiga kura ya kutokuwa na imani naye na kumbadua ofisini.

Barua hiyo hata hivyo imeweka wazi kwamba itamlazima Mwambire kutumia walinzi wa kibinafsi katika kufanikisha usalama wake na wala sio walinzi wanaotambulika na bodi ya bunge la kaunti ya Kilifi.

Haya yamejiri huku Spika Mwambire akipata idhini ya Mahakama kuu ya Malindi kuendelea na majukumu yake ya kikazi kufuatia kesi ambayo iliwasilishwa Mahakamani na wakenya wawili wanaopinga uamuzi wa bunge hilo wa kumtimua ofisini Spika Mwambire.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending