News
Panda shuka za kiuongozi katika serikali za ugatuzi

Huku Kongamano la Ugatuzi awamu ya 12 likiendelea kaunti ya Homa Bay, bado Wakenya wanaendelea kutathmini iwapo malengo ya ugatuzi yanatimizwa.
Yapo maswali mengi tu kuhusu ufanisi wa kimaendeleo na utenda kazi wa serikali za kaunti ambazo hadi sasa nyingi zao zinazidi kulaumiwa kwa kuendeleza ufisadi, usimamizi mbaya wa rasilimali, na utoaji wa huduma duni, suala ambalo limeendelea kuwamulika magavana na maafisa wengine wa serikali za kaunti.
Tangu Ugatuzi uanzishwe baada ya katiba mpya ya mwaka 2010, Bunge la seneti limetenga takribani shilingi trillioni 4 kwa serikali za ugatuzi kupitia mfumo wa ugavi wa rasilimali za serikali kwa huduma za kaunti, ingawa bado kuna maswali mengi kuliko majibu kuhusu malengo yaliyokusudiwa sheria hii ya ugatuzi.
Uongozi wa serikali hizi bado upo kwenye mizani na mitihani mingi tu, ikiwa ni pamoja na ahadi nyingi zinazotolewa na viongozi wa serikali hizi za kaunti ambazo hazitimizwi kutokana na kile wananchi wanadai ni ukiritimba unaotokana na uongozi mbaya, ufisadi na upendeleo katika utoaji wa huduma na kandarasi.
Suala la utoaji wa kandarasi limekuwa donda sugu katika serikali nyingi za kaunti, huku zikiendelea kukabiliwa na malimbikizi ya madeni.
Miongoni mwa sekta zinazotajwa kuathirika zaidi na usimamizi mbaya au ufujaji wa pesa za umma ni sekta ya afya ambayo. Hospitali nyingi hazina dawa huku huduma za afya zikiendelea kudorora kuanzia ngazi za zahanati hadi hospitali kubwa za kaunti.
Serikali za kaunti pia zinashtumiwa kwa kuendelea na uratibu wa miradi hewa katika bajeti zao, na kupelekea kupotea kwa mabilioni ya pesa za uma.
Japo Ugatuzi ulilenga kuboresha maisha ya Wananchi katika ngazi za chini, bado umaskini umekithiri huku mizozo ya uongozi na utawala wa kibepari vikiendelea kushuhudiwa kati ya mabunge ya kaunti na ofisi za magavana.

Wanawake wakichota maji kutokana na manufaa ya ugatuzi {picha kwa hisani}
Matokeo ya mizozo hiyo mara nyingi yamekuwa kushuhudiwa kwa mapinduzi katika usimamizi wa ofisi za magavana kupitia hoja za kutokuwa na Imani nazo, au kutokuwa na Imani na usimamizi wa mabunge ya kaunti na Maspika wa mabunge hayo, hatma yake ikiwa ni kushinikizwa kutimuliwa kutoka ofisi zao.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.
Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.
Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.
Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.
Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.
Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.
Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.
Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
News24 hours ago
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi
-
Sports5 hours ago
Ndoto ya Harambee Stars ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 Yagonga mwamba baada ya kupigwa 3-1 na Gambia Kasarani
-
Sports22 hours ago
Kocha wa Uingereza Thomas Tuchel akataa madai ya “laana” huku akilenga kuvunja ukame wa miaka 60 wa mataji makubwa