Connect with us

Sports

Ojwang Arejea Morans Kwa Msururu Wa Dubai

Published

on

Naibu kocha wa Shujaa Louis Kisia amemtaja winga wa kilabu ya Nakuru Rfc Chrisant Ojwang wakati wa kukitaja kikosi cha Morans kwa ajili ya mashindano ya dunia ya HSBC World Rugby Sevens Series mjini Dubai.

Mchezaji huyo amekua nje kwa zaidi ya miezi saba baada ya kupata jeraha baya la goti ila kwa sasa amepona na yuko tayari kuwakilisha taifa kibarua yake ya kwanza ni kuongoza Kenya kwneye mashindano ya bara Afrika Juni 21-22 nchini Mauritius.

Wachezaji wengine ambayo wametajwa na kocha huyo ni pamoja na Jackson Siketa,Philip Okeya,Felix Okoth,Javan Otieno na Matoka Matoka.

kikosi hicho kiko kundi A pamoja na Uganda, Ivory Coast na Ghana.

Kundi  B kinajumuishwa ,Afrika Kusini,Burkina Faso,Nigeria na Zambia.

Kundi C kinajumisha wenyeji Mauritius,Madagascar,Tunisia na Zimbabwe.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Liverpool Yakubaliana Dili Ya Kerkez

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool imekubaliana na AFC Bournemouth kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 4o kwa beki Milos Kerkez raia wa Serbia.

Tineja huyo anatarajiwa kuwasili Liverpool muda wowote kufanyiwa vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa ligi kuu Uingereza.

Mchezaji huyo alikua nguzo muhimu kwa kilabu ya Bournemouth wakimaliza kumi bora akichangia magoli matano na kufunga mawili,anakua sajili wa tatu kwa kocha Arne Slot kwenye kilabu hio.

The Reds wakiwa wametumia pauni milioni 116 kumpata kiungo Florian Wirtz,pauni milioni 31 kupata Jeremie Frimpong.

Continue Reading

Sports

Starlets Kucheza Fainali Ya CECAFA Dhidi Tanzania

Published

on

By

Kikosi cha soka akina dada kushuka dimbani kucheza dhidi ya Twiga Stars Ya Tanzania kwenye fainali ya kipute cha CECAFA Afrika Mashariki ugani Azam Sports Complex.

Vipusa wa kocha Beldine Odemba wameshinda mechi zote tatu ikiwemo kuwalaza Sudan Kusini magoli 4-0 mechi ya siku ya Alhamisi huku wakiwa wamekusanya alama 9 sawa na wenyeji Tanzania kwenye mashindano ya mwaka huu.

kwa mujibu wa mwalimu huyo wanatarajia mechi ngumu dhidi ya wapinzani wao kwani wako nyumbani na timu bora pia.

“Tuko tayari kwa mechi ya mwisho ambayo pia ni fainali kila mmoja anajua tumekua vizuri katika mashindano haya ila Tanzania ni mpinzani mkubwa katika fainali ya leo kwa sababu pia hawajapoteza mechi kama sisi.”

Mechi hiyo inangoa nanga saa 12.00 jioni.

Continue Reading

Trending