Connect with us

News

Ofisi ya ODPP kufungua mashtaka ya mauaji dhidi ya Masinde

Published

on

Mkurugenzi wa mashtaka ya umma, Renson Ingonga, ameidhinisha mashtaka ya mauaji dhidi ya afisa wa polisi Barasa Masinde.

Masinde anadaiwa kuhusika moja kwa moja na mauaji ya mchuuzi wa barakoa Boniface Kariuki aliyepigwa risasi katikati mwa jiji la Nairobi wakati wa maandamano ya kupinga mauaji ya Albert Ojwang.

Kwenye taarifa iliyotolewa Julai 10, 2025, Ingonga alisema ushahidi uliokusanywa unatosha kufungua kesi ya mauaji dhidi ya afisa huyo wa Polisi, akisisitiza kwamba ni lazima haki ipatikane kwa familia ya marehemu Boniface.

Afisa mwingine aliyekuwa anachunguzwa kwa kuhusika na tukio hilo, Duncan Kiprono, aliondolewa lawama na kuachiliwa huru kwa kukosa ushahidi wa moja kwa moja dhidi yake.

Familia ya marehemu Boniface pamoja na Wanaharakati wa haki za binadamu wamekuwa wakishinikiza haki itendeke, wakitaka wote waliohusika na mauaji ya Boniface wakabiliwe kisheria.

Afisa Masinde anatarajiwa kufikishwa Mahakamani siku zijazo kujibu mashtaka yanayomkabili, huku serikali ikishikilia kwamba maafisa wa polisi wanaokiuka majukumu yao ya kikazi ni lazima wawajibishwe.

Itakumbukwa kwamba Juni 17 mwaka huu wakati wa maandamano ya kupinga mauaji ya Mwanablogu na Mwalimu Albert Ojwang, vurugu zilishuhudiwa katikati mwa jiji la Nairobi na kusababisha baadhi ya vijana wa Gen Z kupoteza maisha yao akiwemo Boniface Kariuki.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending