Connect with us

News

ODM Na PAA, Wafanya mikutano tofauti kuhusu bunge la Kilifi

Published

on

Mikutano miwili muhimu ya faragha imefanyika Jumatatu Juni 2 2025, kujadilia usimamizi wa vyama vya ODM na PAA ndani na nje ya Bunge la Kaunti ya Kilifi.

Taarifa za kuamika zasema, mikutano hiyo miwili ilikusudia kujadili matukio ya hivi majuzi katika Bunge la Kaunti ya Kilifi na usimamizi wake.

Mazungumzo ya Chama cha ODM yaliofanyika mjini Kilifi na kuhudhuriwa na viongozi wote waliochaguliwa, yalijikita katika tetesi za kumtimua Spika wa Bunge Teddy Mwambire, huku kukiwa na mpasuko baina ya wafuasi wa Spika Teddy Mwambire na kwa upande mwengine, wandani wa Gavana Gideon Mung’aro.

Tofauti kubwa za uongozi wa chama hicho cha ODM zilizuka tangu mchakato wa uchaguzi wa mashinani uliotibuka mwaka uliopita na uhasama huo sasa kuelekezwa ndani ya bunge la Kaunti kutaka kumuondoa Spika mamlakani kupitia kura ya kutokuwa na Imani naye ikidaiwa anahujumu serikali ya Gavana Mung’aro.

Pia mkutano huo ulijadili uwezo Mwakilishi Wadi wa Watamu Ibrahim Matumbo wa kuendelea kuwa kiongozi wa wengi Bungeni.

Kuna habari ambazo hazijathibitishwa kwamba huenda chama cha ODM kinataka kumuondoa Ibrahim Matumbo na wadhfa wake kuchukuliwa na Mwakilishi Wadi ya Ganda Oscar Wanje.

Kwa upande mwengine katika mkutano wa Chama cha PAA uliofanyika katika makao makuu ya chama eneo la Nyali kaunti ya Mombasa, yalijikita katika masuala ya usimamizi ndani ya bunge hilo na kumlenga zaidi kiongozi wa walio wachache katika bunge hilo la kaunti Tom Chengo.

Chengo ambaye pia ni Mwakilishi Wadi wa Tezo- kaunti ya Kilifi, anashtumiwa kwa kuhujumu upinzani ndani ya bunge hilo kutokana na usuhuba wake na Gavana Gideon Mung’aro.

Akizungumza na Cocofm kwa njia ya simu, Katibu mkuu wa Chama cha PAA, amnaye pia ni mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu, alikiri kufanyika kwa mkutano huo, siku ya Jumatatu Juni 2, na kwamba mkutano huo ulikuwa kuweka sawa usimamizi na shughuli za chama ndani na nje ya bunge la kaunti.

Katika siku za hivi majuzi bunge hilo limeshuhudiwa mpasuko mkubwa wa kiutawala na kupelekea kutatizwa kwa vikao vya bunge vya kujadili masuala nyeti yanayogusia bejeti na usimamizi wa fedha na utekelezwaji wa miradi katika Wizara ya Afya.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Published

on

By

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.

Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.

Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.

Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.

Taarifa ya Janet Shume

Continue Reading

News

Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya TB

Published

on

By

Kaunti ya Mombasa imetajwa miongoni mwa kaunti zinazoongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu eneo la pwani.

Everlyn Kibuchi mkurugenzi wa mradi wa kuhamasisha kuhusu ungojwa wa kifua kikuu unaofahakima kama Stop TB Project, alitaja mikusanyiko ya watu, ukosefu wa lishe bora na magonjwa ya kuambukiza miongoni mwa vinavyochangia maambukizi ya TB.

Akizungumza katika warsha iliyowaleta pamoja wanahabari jijini Mombasa, Kibuchi alisistiza umuhimu kwa jamii kufahamu dalili za maradhi ya kifua kikuu na kupata matibabu kwa wakati unaofaa.

“Mombasa ni eneo moja ambalo liko na janga kubwa sana la kifua kikuu nchini, changamoto ambayo inafanya kifua kikuu iwe shida zaidi hapa Mombasa ama pwani nimkwamba  Tb inaenea zaidi mahali ambapo kuna mkusanyiko wa watu, kama mtu amepatikana na huo ugonjwa inafaa wale ambao wanaishi nayeye wao pia wanafaa wapimwe kwa sababu kunauwekano kuwa wameambukizwa”, alisema Kibuchi.

Mkurugeniz huyo vile vile alisema unyanyapaa miongoni mwa wanaoishi na ugonjwa wa kifua kikuu umechangia wengi kukosa kufanyiwa vipimo kwa hofu ya kupatikana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.

“Watu wanaogopa kwenda kupimwa kwa sababu wakoishi katika hali ya unyayapaa, wanmajishuku pengine wakipatikana na kifua kikuu watapatikana na maambukizi ya ukimwi, sio watu watote ambao wako na kifua kikuu wanaishi na ukimwi, ni asilimia 23 ya watu Kenya nzima ambao wako na kifua kikuu na ambao wako na ukimwi, hii inamaanisha asilimia 70 hawana virusi”, aliongeza Kibuchi

Kwa upande wake Deche Sanga afisa anayesimamia kitengo cha ugonjwa wa kifua kikuu katika kaunti ya Kilifi, aliweka wazi kwamba waraibu wa dawa za kulevya 5,000 kaunti ya Kilifi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi ya TB, japo wameweka mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.

“Kilifi tuko na takriban waru 5,000 wanaotumia dawa za kulevya, asimilia kubwa ya wanaoishi na TB wanaishi katika haya maeneo ambayo wanavuta unga, hii imefanya Kilifi tumekuja na mbinu ya kudhibiti hili tatizo, tumefungua vituo vya waraibu wa kurekebisha tabia tukishirikiana na wadau wengine, kwa mfano tuko na Omar project Malindi, malengo yake ni kupunguza madhara tukichanganya na HIV”, alisema Sanga.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending