News
Nyanza yavuna Ksh 5.1B baada ya mkutano wa Rais Ruto na viongozi wa Nyanza, Ikulu

Rais William Ruto alikutana na kushauriana na viongozi kutoka eneo la Nyanza katika Ikulu ya Nairobi siku ya Alhamis.
Kulingana na taarifa kutoka Ikulu ya Nairobi, lengo kuu ya mkutano huo lilikiwa ni kutathmini maendeleo yaliyoafikiwa katika eneo la Nyanza.
Katika mkutano na viongozi hao kutoka eneo la Nyaza wakiongozwa na Gavana wa Siaya James Aggrey Orengo, Rais Ruto alisema kwamba serikali imetenga kima cha shilingi bilioni moja kwa ujenzi wa barabara ya Usenge kaunti ya Siaya.
Rais Ruto aliongeza kwamba, mradi huo ni miongoni mwa ile iliyoratibiwa kutekelezwa katika eneo la Nyanza na kutaja upanuzi wa Bandari za sehemu hiyo ili kuboresha biashara na sekta ya Uchumi wa bahari katika eneo hilo la Nyanza.
Katiak taarifa hiyo, Serikali pia itatumia kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kujenga masoko 16 na kiasi, shilingi bilioni 1.6 kufadhili mradi wa kuunganisha umeme kwa zaidi ya familia elfu 16.
Mkutano huu imefanyika siku mbili tu baada ya ziara ya Rais William Ruto katika kaunti ya Homabay ambako aliongoza taifa kuadhimisha sherehe za 62 Madaraka dei Juni, 1 2025.

Picha kwa hisani: Viongozi wa Pwani wakiwa na Rais Ruto Ikulu
Wachanganuzi wa masuala ya kiuchumi walisema ziara hiyo ni mafanikio makubwa kwa juhudi za viongozi wa Siaya, kinyume na ahadi zilizotolewa na serikali wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Ikulu na viongozi kutoka ukanda wa Pwani majuma macha yaliyopita.
Wakati wa mazungumzo hayo na viongozi wa Pwani, Rais Ruto aliahidi kujitolea kwa serikali kuboresha mazingira bora katika kukuza sekta ya Uchumi wa bahari kupitia mikakati ya maendeleo endelevu.
Mengine yaliyozungumzwa wakati wa mkutano huo ni pamoja na juhudi za serikali kumaliza tatizo la Uskwota katika ukanda wa Pwani na usimamizi wa Bandari ya Mombasa.
Mkutano huo ulikuwa umeoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi wa bahari Hassan Ali Joho na mwenzake wa michezo Salim Mvurya.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Ujenzi wa barabara ya Kibaoni-Ganze-Bamba umeng’oa nanga

Baada ya wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kaskazini na Ganze kulalamikia ubovu wa barabara ya Kibaoni-Ganze hadi Bamba na kuangziwa na wanahabari, hali sasa ni tofauti.
Ujenzi wa barabara hiyo iliyoshudia utata na maandamano, sasa unaendelea huku mkandarasi akiwa katika hatua kupiga msasa barabara na kujenga mabomba na sehemu za kupitisha maji hasa kunaponyesha.
Justine Kandie ni muangalizi wa ujenzi wa barabara hiyo, alisema shughuli hiyo imegawanywa mara mbili, na kwa sasa wameanza ujenzi wa barabara hiyo kutoka eneo la Kibaoni mjini Kilifi kuelekea Ganze.
Kandie alisema mpango huo ulianza mwaka 2021 kutoka eneo bunge la Ganze kuelekea kibaoni japo ulisitishwa wakati huo na sasa wameanza tena kujenga umbali wa kilomita tano.
“Katika awamu ya kwanza kwa mwaka wa 2021 tulianza barabara kutoka Ganze tulikuwa tunafanya kilomita tano, kwa mda wa miaka miwili barabara ikasimama kidogo, baadaye kurudi kwa huu mwaka wa 2025 ndio tumepewa kile kiwango tuanze kutoka kibaoni kuelekea Ganze, katika hii awamu ya pili tunafanya kilomita tano ila kwa sababu barabara ni mbovu tumeamua kuanzia huku kwa Kimanje tukielekea Kibaoni ili barabara yetu iwe sawa wakati tunaposafirisha vifaa vya ujenzi”,alisema Kandie.
Baadhi ya mafundi wakiendelea na ujenzi wa barabara ya kuelekea Ganze
Picha:(Joseph Jira)
Kandie pia alisema mda wa miaka miwili aliopewa mkandarasi kukamilisha ujenzi huo wa barabara utategemea na mgao wa pesa zitatakaotolewa kufanikisha mradi huo.
“Ule mda wa kukamilisha barabara huwa inategemea uwezo wa mwanakandarasi kama ako na fedha za kutosha, itamsaidia kukamilisha kwa mda unaofaa, kwa sababu hii barabara yetu walikuwa wametupa kama miaka miwili ila saa hii mda umesonga”, aliongeza Kandie.
Wakaazi pamoja na wahudumu wa uchukuzi wa umma wanaotumia barabara hiyo wameeleza matumaini ya kuimarika kwa sekta ya uchukuzi sawa na uchumi mara tu ujenzi utakapokamilika.
Itakumbukwa kwamba barabara hiyo ilileta utata na kusababisha wakaazi kuandamana na kuifunga sawa na kutatiza shughuli za usafiri kwa mda.
“Hapo kwa usafiri na biashara huenda kukabadilika kwa sababu wengi pia wanakataa huku kwa sababu yah ii barabara vile ni mbovu hasa kazi zinakuwa ziko chini kwa sababu ya vumbi”,alisema Jeremiah Mwaringa
Tinga tinga za ujenzi wa barabara ya kuelekea Ganze.
Picha:(Joseph Jira)
Mvutano huo pia ulishuhudiwa baina ya mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu Tungule na mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya kuhusu ujenzi wa barabara unakofaa kuanza kutekelezwa.
Hata hivyo muangalizi wa mradi huu aelieleza matumaini yake kuwa mvutano huo wa wanasiasa hautaathiri utendakazi wao huku akishinikiza wahudumu wa barabara hiyo kuwa na uvumilivu wakati wanapoendelea na ujenzi huo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.
Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.
Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.
Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.
Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.
Taarifa ya Janet Shume