News
Nyanza yavuna Ksh 5.1B baada ya mkutano wa Rais Ruto na viongozi wa Nyanza, Ikulu

Rais William Ruto alikutana na kushauriana na viongozi kutoka eneo la Nyanza katika Ikulu ya Nairobi siku ya Alhamis.
Kulingana na taarifa kutoka Ikulu ya Nairobi, lengo kuu ya mkutano huo lilikiwa ni kutathmini maendeleo yaliyoafikiwa katika eneo la Nyanza.
Katika mkutano na viongozi hao kutoka eneo la Nyaza wakiongozwa na Gavana wa Siaya James Aggrey Orengo, Rais Ruto alisema kwamba serikali imetenga kima cha shilingi bilioni moja kwa ujenzi wa barabara ya Usenge kaunti ya Siaya.
Rais Ruto aliongeza kwamba, mradi huo ni miongoni mwa ile iliyoratibiwa kutekelezwa katika eneo la Nyanza na kutaja upanuzi wa Bandari za sehemu hiyo ili kuboresha biashara na sekta ya Uchumi wa bahari katika eneo hilo la Nyanza.
Katiak taarifa hiyo, Serikali pia itatumia kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kujenga masoko 16 na kiasi, shilingi bilioni 1.6 kufadhili mradi wa kuunganisha umeme kwa zaidi ya familia elfu 16.
Mkutano huu imefanyika siku mbili tu baada ya ziara ya Rais William Ruto katika kaunti ya Homabay ambako aliongoza taifa kuadhimisha sherehe za 62 Madaraka dei Juni, 1 2025.

Picha kwa hisani: Viongozi wa Pwani wakiwa na Rais Ruto Ikulu
Wachanganuzi wa masuala ya kiuchumi walisema ziara hiyo ni mafanikio makubwa kwa juhudi za viongozi wa Siaya, kinyume na ahadi zilizotolewa na serikali wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Ikulu na viongozi kutoka ukanda wa Pwani majuma macha yaliyopita.
Wakati wa mazungumzo hayo na viongozi wa Pwani, Rais Ruto aliahidi kujitolea kwa serikali kuboresha mazingira bora katika kukuza sekta ya Uchumi wa bahari kupitia mikakati ya maendeleo endelevu.
Mengine yaliyozungumzwa wakati wa mkutano huo ni pamoja na juhudi za serikali kumaliza tatizo la Uskwota katika ukanda wa Pwani na usimamizi wa Bandari ya Mombasa.
Mkutano huo ulikuwa umeoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi wa bahari Hassan Ali Joho na mwenzake wa michezo Salim Mvurya.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Wahudumu wa afya Lamu watishia kuishtaki serikali ya kaunti hiyo

Wahudumu wa Afya kaunti ya Lamu wametishia kuelekea Mahakamani kuishtaki serikali ya kaunti hiyo kwa kukaidi kutekeleza matakwa yao.
Wahudumu hao waliishtumu serikali ya kaunti ya Lamu kwa kupuuza matakwa yao na badala yake kutumia vitisho ili kuwashurutisha kurejea kazini.
Kulingana na viongozi wa wahudumu hao, licha ya mgomo wao kuendelea kwa zaidi ya wiki mbili serikali ya kaunti hiyo imekataa kata kuandaa vikao vya kusuluhisha malalamishi yao.
Baadhi ya changamoto wanazolalamikia ni pamoja na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 10 bila ya kupandishwa vyeo, kupuuzwa kwa mkataba wa makubaliano ya nyongeza ya mishahara, kunyimwa kwa mishahara kwa baadhi ya wahudumu hao miongoni mwa matakwa mengine.
“Mkiendelea kutufinyilia itabidi tufuate njia ya sheria kwa sababu tunajua tunalilia haki yetu, haiwezekani serikali ya kaunti inashindwa kutupandisha vyeo ilhali tumefanya kazi kwa miaka 15 sasa, hatuwezi kuendelea kufanya kazi katika mazingira duni na pia mkataba wa makubaliano kuhusu nyongeza ya mishahara sharti itekelezwe” walisisitiza viongozi hao.
Wakati uo huo serikali ya kaunti ya Lamu imejibu malimishi yao kupitia barua na kutangaza kuwa mgomu huo ni kinyume cha seria na kuwataka wahudumu hao kurejea kazini mara moja.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Rais Ruto atuma KDF kusimamia ujenzi wa hospitali nchini

Rais William Ruto ametuma jeshi la KDF kusimamia ujenzi wa vituo vya afya zaidi ya 75 kote nchini katika juhudi za kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa haraka.
Akizungumza katika kaunti ya Narok wakati wa uzinduzi wa hospitali ya Sogoo Level 4, waziri wa ulinzi Patrick Mariru alifichua kuwa ujenzi wa hospitali hiyo yenye mamlaka kamili itakamilika baada ya mda wa miezi 11.
Ujenzi wa hospitali ya Sogoo Level 4 ulivutia rais Ruto alipozuru eneo hilo mwezi mei mwaka 2025, jambo lililomfanya kuagiza KDF kuipandisha hadhi.
Mariru hata hivyo alishikilia kuwa wafanyikazi wote wasio na ujuzi watatolewa kutoka kwa jamii.
“Jeshi litamsimamia mkandarasi. Hilo liwe wazi, kazi yote itafanywa na vijana wa Sogoo. Tutaweka maafisa wawili na kila jioni watanipa ripoti ya maendeleo,” alisema Mariru.
“Tuna zaidi ya miradi 75 tunayosimamia na sio kwamba tunabadilisha wakala wa serikali tunataka tu kushirikiana na ofisi tofauti miongoni mwao wizara za afya na michezo.”
Taarifa ya Joseph Jira