Connect with us

News

Nyanza yavuna Ksh 5.1B baada ya mkutano wa Rais Ruto na viongozi wa Nyanza, Ikulu

Published

on

Rais William Ruto alikutana na kushauriana na viongozi kutoka eneo la Nyanza katika Ikulu ya Nairobi siku ya Alhamis.

Kulingana na taarifa kutoka Ikulu ya Nairobi, lengo kuu ya mkutano huo lilikiwa ni kutathmini maendeleo yaliyoafikiwa katika eneo la Nyanza.

Katika mkutano na viongozi hao kutoka eneo la Nyaza wakiongozwa na Gavana wa Siaya James Aggrey Orengo, Rais Ruto alisema kwamba serikali imetenga kima cha shilingi bilioni moja kwa ujenzi wa barabara ya Usenge kaunti ya Siaya.

Rais Ruto aliongeza kwamba, mradi huo ni miongoni mwa ile iliyoratibiwa kutekelezwa katika eneo la Nyanza na kutaja upanuzi wa Bandari za sehemu hiyo ili kuboresha biashara na sekta ya Uchumi wa bahari katika eneo hilo la Nyanza.

Katiak taarifa hiyo, Serikali pia itatumia kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kujenga masoko 16 na kiasi, shilingi bilioni 1.6 kufadhili mradi wa kuunganisha umeme kwa zaidi ya familia elfu 16.

Mkutano huu imefanyika siku mbili tu baada ya ziara ya Rais William Ruto katika kaunti ya Homabay ambako aliongoza taifa kuadhimisha sherehe za 62 Madaraka dei Juni, 1 2025.

Picha kwa hisani: Viongozi wa Pwani wakiwa na Rais Ruto Ikulu

Wachanganuzi wa masuala ya kiuchumi walisema ziara hiyo ni mafanikio makubwa kwa juhudi za viongozi wa Siaya, kinyume na ahadi zilizotolewa na serikali wakati wa mazungumzo yaliyofanyika Ikulu na viongozi kutoka ukanda wa Pwani majuma macha yaliyopita.

Wakati wa mazungumzo hayo na viongozi wa Pwani, Rais Ruto aliahidi kujitolea kwa serikali kuboresha mazingira bora katika kukuza sekta ya Uchumi wa bahari kupitia mikakati ya maendeleo endelevu.

Mengine yaliyozungumzwa wakati wa mkutano huo ni pamoja na juhudi za serikali kumaliza tatizo la Uskwota katika ukanda wa Pwani na usimamizi wa Bandari ya Mombasa.

Mkutano huo ulikuwa umeoongozwa na Waziri wa madini na Uchumi wa bahari Hassan Ali Joho na mwenzake wa michezo Salim Mvurya.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kongamano la mabadiliko ya hali ya anga lafanyika Mombasa

Published

on

By

Mratibu wa Kongamano la kimataifa linaloangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga, INTER- GOVERNMEMTAL PANEL ON CLIMATE CHANGE, Patricia Nying’uro amesema jamii inasalia kuwa kiungo muhimu katika harakati za kuangazia mfumo wa mabadiliko ya hali ya hewa.

Kufuatia hilo, Nying’uro alitoa wito kwa wadau wa mazingira kuwekeza zaidi na kuhakikisha kila mmoja anashiriki ipasavyo katika kudhibiti mabadiliko hayo.

Nying’uro alisema Kongamano ambalo linaendelea katika kaunti ya Mombasa, linaangazia masuala ya mabadiliko ya hali ya anga na limewekeza kutambuliwa na jamii katika mikakati hiyo.

Akizungumza katika eneo la Shanzu wakati wa majadiliano hayo, Nying’uro alisema jumla ya mataifa 56 kati ya mataifa 195 yanayoshiriki kwenye mchakato wa kuweka mipango, sera na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa yanakongamana eneo la Shanzu ili kuanisha ripoti ambayo itatoa muongozo rasmi wa kuangazia makali ya mabadiliko ya hali ya hewa.

Wakati huohuo, Nying’uro alisema pia kongamano hilo la kimataifa lina umuhimu mkubwa kwa taifa hili kwani Kenya itahusishwa moja kwa moja katika kupangilia sera za kimataifa za kudhibiti athari ya mabadiliko ya hali ya anga.

Taarifa ya Janet Shume

Continue Reading

News

Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya TB

Published

on

By

Kaunti ya Mombasa imetajwa miongoni mwa kaunti zinazoongoza kwa maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu eneo la pwani.

Everlyn Kibuchi mkurugenzi wa mradi wa kuhamasisha kuhusu ungojwa wa kifua kikuu unaofahakima kama Stop TB Project, alitaja mikusanyiko ya watu, ukosefu wa lishe bora na magonjwa ya kuambukiza miongoni mwa vinavyochangia maambukizi ya TB.

Akizungumza katika warsha iliyowaleta pamoja wanahabari jijini Mombasa, Kibuchi alisistiza umuhimu kwa jamii kufahamu dalili za maradhi ya kifua kikuu na kupata matibabu kwa wakati unaofaa.

“Mombasa ni eneo moja ambalo liko na janga kubwa sana la kifua kikuu nchini, changamoto ambayo inafanya kifua kikuu iwe shida zaidi hapa Mombasa ama pwani nimkwamba  Tb inaenea zaidi mahali ambapo kuna mkusanyiko wa watu, kama mtu amepatikana na huo ugonjwa inafaa wale ambao wanaishi nayeye wao pia wanafaa wapimwe kwa sababu kunauwekano kuwa wameambukizwa”, alisema Kibuchi.

Mkurugeniz huyo vile vile alisema unyanyapaa miongoni mwa wanaoishi na ugonjwa wa kifua kikuu umechangia wengi kukosa kufanyiwa vipimo kwa hofu ya kupatikana na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ukimwi.

“Watu wanaogopa kwenda kupimwa kwa sababu wakoishi katika hali ya unyayapaa, wanmajishuku pengine wakipatikana na kifua kikuu watapatikana na maambukizi ya ukimwi, sio watu watote ambao wako na kifua kikuu wanaishi na ukimwi, ni asilimia 23 ya watu Kenya nzima ambao wako na kifua kikuu na ambao wako na ukimwi, hii inamaanisha asilimia 70 hawana virusi”, aliongeza Kibuchi

Kwa upande wake Deche Sanga afisa anayesimamia kitengo cha ugonjwa wa kifua kikuu katika kaunti ya Kilifi, aliweka wazi kwamba waraibu wa dawa za kulevya 5,000 kaunti ya Kilifi wako katika hatari ya kuambukizwa maradhi ya TB, japo wameweka mikakati ya kukabiliana na hali hiyo.

“Kilifi tuko na takriban waru 5,000 wanaotumia dawa za kulevya, asimilia kubwa ya wanaoishi na TB wanaishi katika haya maeneo ambayo wanavuta unga, hii imefanya Kilifi tumekuja na mbinu ya kudhibiti hili tatizo, tumefungua vituo vya waraibu wa kurekebisha tabia tukishirikiana na wadau wengine, kwa mfano tuko na Omar project Malindi, malengo yake ni kupunguza madhara tukichanganya na HIV”, alisema Sanga.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending