Sports
Noni Madueke Atua Arsenal

Sasa ni Rasmi Noni Madueke ni mali ya Arsenal vilabu vyote viwili vimekubaliana kwa ajili ya uhamisho huo wa pauni milioni 52 dhidi ya Muingereza huyo.
Mchezaji huyo anatarajiwa kuwasili mjini London kwa ajili ya vipimo vya kiafya kabila ya kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na wanabunduki hao wa London Kaskazini.
Madueke mwenye umri wa miaka 23 anakua sajili wa nne kwa kocha Mikel Arteta baada ya kuwasili kwa kipa Kepa Arrizabalaga, kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi na kiungo Christian Norgaard kutoka Brenford.
Nyota huyo amekua na kilabu ya The Blues nchini Marekani kwa kombe la Dunia baina ya vilabu huku akiacha kilabu yake ikijianda kwa fainali Jumapili hii.
Continue Reading
Sports
Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Sports
Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.