Connect with us

News

NGEC, yasisitiza udhibiti wa dhulma za kijinsia

Published

on

Tume ya jinsia na usawa NGEC inasisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wanaume ili kudhibiti visa vya dhuluma za kijinsia nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mkakati wa miaka mitano ya tume hiyo, Waziri wa jinsia nchini Hanna Cheptumo alisikitishwa na ongezeko la visa vya ukatili wa kijinsia na kusisitiza umuhimu wa kuwahusisha vijana na watu walio na uatilifu ili kudhibiti dhuluma mbalimbali na kuleta usawa katika jamii.

Vile vile, Cheptumo alishinikiza uwekezaji kwenye miradi ya kuwawezesha kiuchumi wanawake, watu walio na uatilifu na vijana.

Cheptumo alisema iwapo watu walio na uatilifu, vijana na wanawake watawezeshwa ipasavyo wataweza kujikimu kimaisha na hata familia zao bila kutegemea misaada na kusisitiza kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kubaguliwa kwa namna yoyote ile.

“Kifungu cha 27 cha Katiba ya nchi ya mwaka wa 2010, inampa kila mtu haki ya usawa na uhuru dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote’’ Alisema Cheptumo.

Kwa upande wake msemaji wa serikali Isaac Mwaura alitoa wito kwa watu walio na uatilifu kuweka juhudi zaidi katika kujiendeleza kimaisha badala ya kusubiri msaada kutoka kwa mashirika mbalimbali na serikali huku akiwataka kujikubali na kupuuza yale ambayo yanasemwa kuhusu hali zao kwani wana uwezo kama wanadamu wengi.

“Kama watu walio na uatilifu mtapitia unyanyapaa mwingi kutoka kwa watu hasa mnapopata nafasi za uongozi kwa sababu kuna watu wanaona hamstahili’’ alisema Mwaura.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending