Connect with us

News

NGEC, yasisitiza udhibiti wa dhulma za kijinsia

Published

on

Tume ya jinsia na usawa NGEC inasisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wanaume ili kudhibiti visa vya dhuluma za kijinsia nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mkakati wa miaka mitano ya tume hiyo, Waziri wa jinsia nchini Hanna Cheptumo alisikitishwa na ongezeko la visa vya ukatili wa kijinsia na kusisitiza umuhimu wa kuwahusisha vijana na watu walio na uatilifu ili kudhibiti dhuluma mbalimbali na kuleta usawa katika jamii.

Vile vile, Cheptumo alishinikiza uwekezaji kwenye miradi ya kuwawezesha kiuchumi wanawake, watu walio na uatilifu na vijana.

Cheptumo alisema iwapo watu walio na uatilifu, vijana na wanawake watawezeshwa ipasavyo wataweza kujikimu kimaisha na hata familia zao bila kutegemea misaada na kusisitiza kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kubaguliwa kwa namna yoyote ile.

“Kifungu cha 27 cha Katiba ya nchi ya mwaka wa 2010, inampa kila mtu haki ya usawa na uhuru dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote’’ Alisema Cheptumo.

Kwa upande wake msemaji wa serikali Isaac Mwaura alitoa wito kwa watu walio na uatilifu kuweka juhudi zaidi katika kujiendeleza kimaisha badala ya kusubiri msaada kutoka kwa mashirika mbalimbali na serikali huku akiwataka kujikubali na kupuuza yale ambayo yanasemwa kuhusu hali zao kwani wana uwezo kama wanadamu wengi.

“Kama watu walio na uatilifu mtapitia unyanyapaa mwingi kutoka kwa watu hasa mnapopata nafasi za uongozi kwa sababu kuna watu wanaona hamstahili’’ alisema Mwaura.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mvuvi aliyezama baharini Watamu apatikana Tanariver

Published

on

By

Mwili wa mvuvi Hudhefa Laly aliyepotea baharini huko Watamu eneo bunge la Kilifi Kaskazini Kaunti ya Kilifi akiwa na ndugu yake Athman Laly umepatikana eneo la Shakiko -Mathole, kaunti ya Tana River.

Ndugu hao wawili walitoweka habarini siku ya Alhamisi 24, Julai 2025 katika bahari hindi wakati wakiendelea na shughuli zao za uvuvi.

Vitengo mbali mbali vya uokozi vimekuwa vikiendesha zoezi la kutafuta miili ya wawili hao kwa ushirikiano na wavuvi eneo la Watamu.

Kufikia sasa mwili wa Athman Laly kakake Hudhefa ungali haujapatikana huku juhudi za kuutafuta zikiendelea.

Jamii ya wavuvi katika eneo la Watamu ikiongozwa na kiongozi wa vijana Bakari Shaban iliiomba serikali ya kaunti ya Kilifi na ile ya kitaifa kununua boti za uokozi ili kusaidia kuokoa maisha wakati kunapotokea dharura baharini.

“Tunaomba tupate boti za kuokoa maisha baharini, popote alipo waziri Ali Joho angalau tupate boti za uokozi kama mbili hapa Watamu ni kitovu cha utalii kunamahoteli mengi, watalii wote wanaokuja Watamu mpaka leo hakuna boti za uokozi”, alisema Shaban.

Awali wao wazazi wa wavuvi waliopotea baharini Lali Athman Lali na Dhurai Mohamed Ali waliiomba serikali kuweka juhudi zaidi za kuwasaidia kuwapata wanawao kwani ndio tegemeo kubwa kwa familia yao.

“Uko usaidizi unatumika, kuna vijana wanaojitolea kwa maboti wanaenda ile sehemu ambayo wavuvi wanavua, wanajaribu kuzunguka lakini toka siku hiyo hawajapata chochote: Katika Maisha yangu mimi nawategemea hawa watoto kunisomeshea hawa watoto wangu ambao ni wadogo zao mashule, kwa chakula kwa hivyo naomba serikali inisaidie kwa sababu ndio tegemeo langu hao watoto”.walisema wazazi.

Kisa hiki kilijiri miezi kadhaa baada ya mvuvi mmoja kutoka eneo la Mnarani mjini Kilifi kufariki baharini baada ya kugongwa kichwani kwa pondo na wavuvi wenzake kulipotokea mzozo kuhusu pato la samaki.

Kufikia sasa mwili wa mvuvi huyo haujapatikana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mombasa inaongoza kwa maambukizi ya MPOX nchini

Published

on

By

Wizara ya afya nchini imesema kaunti ya Mombasa inaongoza kwa visa vya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa idara ya afya nchini Daktari Patrick Amoth, kaunti ya Mombasa imerekodi visa 139 kati ya visa 300 vilivyoripotiwa na wizara hiyo.

Amoth alidokeza kuwa serikali itatangaza siku maalum ya kutoa chanjo ya kudhibiti msambao wa ugonjwa huo wakishirikiana na shirika la afya ulimwenguni WHO.

Mkurugenzi huyo vile vile alimesema zoezi hilo litaambatana na hamasa kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi zaidi.

“Kwa wakati huu Mombasa ndio inaongoza kwa idadi ya visa 139 kwa hivyo tuchuke tahadhari kuhakikisha kwamba tunazuia maambukizi, na tunafanya mpango pamoja na shirika la afya duniani WHO, hapa tutakuja na mpango wa chanjo na ikifika huo wakati tunaomba watu wajitokeze wapate chanjo ili wapate kinga”,alisema Daktari Amoth.

Wakati huo huo Amoth aliokeza kuwa uchunguzi wa vifo vya watu wanne walioaga dunia wiki chache zilizopita huko Migadini, eneo bunge la Changamwe kaunti ya Mombasa umebaini walifariki kutokana na magonjwa mengine na wala sio maambukizi ya ugonjwa wa MPOX kama ilivyodhaniwa na wakaazi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending