Connect with us

News

Mzugha, awahimiza vijana kaunti ya Taita taveta kuzingatia elimu

Published

on

Mwakilishi wa wadi ya Mbololo kaunti ya Taita taveta Lawrence Mzugha ametoa wito kwa vijana katika eneo hilo kuzingatia elimu.

Kulingana na Mzugha kuna nafasi nyingi za ajira ikiwemo uendeshaji bodaboda, magari miongoni mwa fursa nyingine za kujikimu kimaisha ambazo zinahitaji ujuzi.

Aidha, Mzugha aliahidi kuwaunga mkono vijana wa wadi yake wanaonuia kupata ujuzi kupitia ufadhili unaotolewa na serikali ikiwemo basari na michango mingine katika jamii hasa ule wa kufadhili elimu.

“Kwa uwezo wa Mungu kuna baadhi ya vitu ambavyo nimefanya, maana kwa elimu muswada wa kwanza kuingia bungeni kuhusu elimu, mimi ndio nilipeleke’’, alisema Mzugha.

Mzugha alisema fomu za basari katika wadi hiyo ya Mbololo zinapatikana kwa mtandao.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC yasistiza usalama kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu

Published

on

By

Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, Erastus Ethekon, amesisitiza umuhimu wa usalama katika maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2027.

Akizungumza kwenye mkutano wa ushirikiano na vitengo vya usalama kutoka kaunti za Mombasa, Kwale na Kilifi, Ethekon alisema tume ya IEBC imeendelea kushirikiana kwa karibu na vitengo hivyo tangu mwaka 2013, kuhakikisha chaguzi zinakuwa za amani, haki na uwazi.

Hata hivyo Ethekon alikiri kuwepo kwa changamoto kama vile uhaba wa fedha, vitisho vipya vya kiusalama, ukiukaji wa haki za binadamu, pamoja na ghasia za kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana wakati wa chaguzi.

Mwenyekiti huyo vile vile alisema usalama wa uchaguzi si wa siku ya kupiga kura pekee, bali ni mchakato unaopaswa kuzingatiwa kuanzia usajili wa wapiga kura hadi kutangazwa kwa matokeo.

Kwa upande wake, kamishna wa IEBC Anne Nderitu alisema tume ya IEBC imeweka mikakati kuhakikisha chaguzi ndogo zipatazo 24, zinafanyika kwa uwazi na kwa kuzingatia sheria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending