News
Murkomen: Polisi kupokea nyongeza ya mshahara

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema serikali inalenga kufanikisha nyongeza ya mishahara ya maafisa wa polisi kote nchini kwa asilimia 10.
Waziri Murkomen alisema mpango huo utatekelezwa kwa awamu na kwa kuambatana na bajeti ya serikali ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026 ili kuwapa motisha maafisa wa polisi na kufanikisha utendakazi bora.
Akizungumza katika kaunti ya Nandi wakati wa kikao cha baraza la usalama maarufu Jukwaa la usalama, Waziri Murkomen aliwataka maafisa wa polisi kuwa na subra wakati suala hilo linaposhughulikiwa.
“Serikali iko na mpango maalum wa kuhakikisha maaskari wetu wanapokea nyongeza ya mishahara kwa asilimia 10 na hii ni kuhakikisha tunawapa motisha maafisa wetu wa usalama na nitekelezwa kupitia Ofisi ya huduma ya polisi nchini na ile ya Inspekta jenerali wa polisi”, alisema Murkomen.
Waziri Murkomen alidokeza kwamba tatizo la majangili katika maeneo ya Pokot Magharibi, Turkana, Samburu, Baringo, na Elgeyo Markwet kama changamoto kuu ya kiuslama katika maeneo ya Bonde la Ufa, akisema serikali inafuatilia kati ya bunduki haramu elfu 5 hadi elfu 10 zinazomilikiwa na majangali.
“Tuko na tatizo kubwa katika maeneo ya bonde la Ufa hasa Pokot Magharibi na kule Baringo na Samburu lakini tumejipanga kama idara ya usalama tutahakikisha kumesambaratisha hao majangili na kurudisha bundiki zote haramu ambazo wanatumia kuhangaisha watu”, alieleza Murkomen.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.
Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.
Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.
Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.
Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.
Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.
Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.
Taarifa ya Joseph Jira.
News
Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.
Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.
Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.
Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.
Taarifa ya Joseph Jira.