Connect with us

News

Murkomen: Polisi kupokea nyongeza ya mshahara

Published

on

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema serikali inalenga kufanikisha nyongeza ya mishahara ya maafisa wa polisi kote nchini kwa asilimia 10. 

Waziri Murkomen alisema mpango huo utatekelezwa kwa awamu na kwa kuambatana na bajeti ya serikali ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026 ili kuwapa motisha maafisa wa polisi na kufanikisha utendakazi bora.

Akizungumza katika kaunti ya Nandi wakati wa kikao cha baraza la usalama maarufu Jukwaa la usalama, Waziri Murkomen aliwataka maafisa wa polisi kuwa na subra wakati suala hilo linaposhughulikiwa.

“Serikali iko na mpango maalum wa kuhakikisha maaskari wetu wanapokea nyongeza ya mishahara kwa asilimia 10 na hii ni kuhakikisha tunawapa motisha maafisa wetu wa usalama na nitekelezwa kupitia Ofisi ya huduma ya polisi nchini na ile ya Inspekta jenerali wa polisi”, alisema Murkomen.

Waziri Murkomen alidokeza kwamba tatizo la majangili katika maeneo ya Pokot Magharibi, Turkana, Samburu, Baringo, na Elgeyo Markwet kama changamoto kuu ya kiuslama katika maeneo ya Bonde la Ufa, akisema serikali inafuatilia kati ya bunduki haramu elfu 5 hadi elfu 10 zinazomilikiwa na majangali.

“Tuko na tatizo kubwa katika maeneo ya bonde la Ufa hasa Pokot Magharibi na kule Baringo na Samburu lakini tumejipanga kama idara ya usalama tutahakikisha kumesambaratisha hao majangili na kurudisha bundiki zote haramu ambazo wanatumia kuhangaisha watu”, alieleza Murkomen.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending