Connect with us

Sports

MTG United Wana Malengo ya Kucheza Ligi Kuu

Published

on

Mkufunzi wa kilabu ya akina Dada ya Moving The Goal Post marufu kama MTG United kaunti hii ya Kilifi Fadhili Hamisi marufu coach Tibo amesema kwamba wanalenga kushiriki ligi ya FKFWPL siku za usoni.

Kwenye mahojiano ya kipekee na Kipenga Cha CoCo FM mwalimu huyo ana imani wa kikosi Bora kutimiza malengo hayo. “Nataka MTG United iwe timu ya kwanza ya akina Dada kaunti ya Kilifi kushiriki ligi ya akina Dada nchini kwani Wana uwezo huo.

“Aidha mwalimu huyo amesema licha ya changamoto chungu nzima wanazokumbana za kifedha Lengo lao si kuona tu timu hiyo inapaa Bali pia kuona badhi ya akina Dada hao wanacheza ligi za ndaani na nje za nchi siku za usoni. “Ni wasichana ambao Wana Vipaji itafurahisha sana wakicheza ligi ya ndaani na nje ya nchi hii siku za badaye.

“Vilevile mwalimu huyo ameongezea licha ya Soka akina Dada hao wanapewa mafunzo mengine ikiwemo jinsi ya kuishi vizuri katika jamii,msongo wa mawazo miongoni mwa mengine.

“MTG United haideal tu na soka tuko na vitengo vingine vya kuisaidia makuzi ya mtoto wa kike kama kujitambua katika jamii wanapoingia wakiwa wachanga kuanzia umri wa miaka 9-25.

” MTG United yenye makao hapa mnarani iko nafasi ya Saba ligi ya Supa baada ya kushiriki mechi 15.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Taifa Ya DR Congo Yawasili Nchini Kwa Mechi Ya Ufunguzi Dhidi Ya Harambee Stars

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo) imewasili nchini mapema leo kwa ajili ya mechi ya ufunguzi dhidi ya Harambee Stars itakayochezwa siku ya Jumapili.

Kikosi hicho, kilicho na wachezaji 25 pamoja na benchi la kiufundi, kiliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) na kupokelewa rasmi kabla ya kuelekea hotelini jijini Nairobi.

DR Congo, maarufu kama The Leopards, ni mabingwa mara mbili wa kombe hilo na wanatarajiwa kufanya mazoezi yao ya kwanza jioni ya leo katika Uwanja wa Kasarani.

Vijana hao wako katika Kundi A pamoja na wenyeji Kenya, pamoja na AngolaMorocco, na Zambia.

Continue Reading

Sports

Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Published

on

By

SIKU 3 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN:
Waziri wa Michezo, Salim Mvurya, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya CHAN, Nicholas Musonye, wamefanya ukaguzi wa mwisho leo katika viwanja vya Kasarani na Nyayo kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Harambee Stars na DR Congo itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Kasarani.

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.

Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.

Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.

Continue Reading

Trending