Connect with us

Entertainment

Msanii Ndiye Amezaa Mwanaharakati, Chibo Dee Avunja Ukimya

Published

on

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Chibo Dee amevunja ukimya na kueleza kwa kina sababu zilizompelekea kuonekana kuisifu serikali, akijibu kwa hisia ukosoaji kutoka kwa blogger aliyemhoji kama ni “msanii, mwanaharakati ama chawa wa wanasiasa?”

Katika ujumbe aliouandika kupitia Facebook, Chibo Dee alifunguka kuhusu safari yake ya sanaa iliyojaa mapambano, akieleza kuwa kabla ya watu kumwelewa vibaya leo, alikuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za wananchi kupitia kazi yake ya muziki.

“Msanii ndiye amezaa mwanaharakati. Back in 2019 August, nilipokuwa naendeleza harakati za kutetea mwananchi na kukosoa serikali nilikuwa peke yangu. Nilitumia sanaa kuonyesha haki na bora ila nilijikuta matatani kwa kupelekwa polisi. Ila nilitolewa na wanasiasa. Wiki mbili ukiwa locker 😭😭😭.”

Chibo Dee anasema kuwa aliwahi kupitia wakati mgumu, ambapo harakati zake zilimpeleka rumande kwa zaidi ya wiki mbili. Kulingana naye, ni msaada wa kisiasa uliomtoa kutoka hali hiyo – jambo ambalo sasa linafanya wengine kumtazama tofauti.

Ujumbe huo ni jibu la moja kwa moja kwa blogger ambaye awali aliandika: “Chawa, Mwanaharakati au Msanii? – Chibo Dee,”  akiambatanisha picha ya msanii huyo, hatua iliyozua mjadala mkali mitandaoni.

Lakini kwa waliofuatilia safari ya Chibo Dee tangu mwaka 2019, ujumbe wake unadhihirisha kuwa sanaa kwake haikuwa tu burudani – bali chombo cha kupigania haki, na njia ya kuwasemea wasio na sauti.

Mara baada ya taarifa hiyo kusambaa, wafuasi na watumiaji wa mitandao walijitokeza na kutoa maoni yao. Baadhi walimtetea Chibo Dee, huku wengine wakionekana kumtupia lawama au dhihaka.

Maico Charly KE:
“Inawauma nini kwani si ni maisha yake… watu wengine bhana… mtandaoni kutwa kufuatilia watu tu!”

Kensam Kijazo:
“Njaaa inamsumbua, muacheni apate mkate wake.”

Nicko Wangu:
“Chibo Dee, piga kazi mwanangu. Chawa sio wewe – admin ndiye kibaraka wa Asha Jumwa, uwe mwelewa mdogo wangu!”

Chibo Dee ni miongoni mwa waimbaji waliotumbuiza waombolezaji kwenye mazishi ya babake gavana wa kaunti ya Kilifi, Gideon Maitha Mung’aro, Gideon Baya Mung’aro aliyeaga dunia mwezi Juni 15, 2025.

Mazishi hayo yalifanyika wadi ya Dabaso, Kilifi Kaskazini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Sijakataa Kuchangiwa, Ila Nipewe Heshima, Nyevu Fondo Afunguka

Published

on

Muunda maudhui maarufu Pwani, Nyevu Fondo, amefunguka sababu zake za kukataa pesa za mchango wa matibabu zilizochangishwa na Presenter Jakki.

Presenter Jakki, bila kumjulisha Nyevu, alianzisha kampeni ya mchango wa matibabu kwa jina lake baada ya kujua Nyevu anaugua, akiwahamasisha mashabiki na wafuasi wake kutuma msaada wa fedha akishiriki picha za Nyevu Fondo kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza hewani kwenye kipindi cha Janjaruka 254, Nyevu alisema wazi kuwa hana tatizo na watu kumchangia, lakini alikerwa na jinsi jambo hilo lilivyofanywa bila ushauriano:

“Mimi sijakataa kuchangiwa. Ni kitu poa. Kitu ambacho kinaniumiza ni kuwa kwa nini hakuniuliza mimi mwenyewe, naugua nini na nahitaji msaada aina  gani? Je, ule ugonjwa unahitaji msaada wa aina gani ama kile kitu nachougua kinahitaji msaada ama ala?”

Awali kwenye ukurasa wake wa Facebook Nyevu Fondo aliandika;

“Presenter Jacky, natumai uko salama dadangu. Kwanza, nashukuru kwa jitihada zako na za followers wako kunichangia – ni ishara ya upendo na utu. Lakini ujumbe wangu kwako ni huu: kabla ya kuchukua hatua kama hiyo tena, tafadhali niulize mimi binafsi kwanza. Wazo lako lilikuwa zuri upande wako, lakini kwangu halikukaa vizuri kwa sababu sikupewa nafasi kueleza hali yangu. Kwa sasa, sina uhitaji wa mchango huo kwani ninao msaada kutoka kwa Betty Kache Mwavuo, Hon. Oscar Wanje, na baadhi ya followers wanaonijali kama Mche Mtsumi na wengine wa Team Gulf.”

Hata hivyo Presenter Jakki hajanyamaza. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Jakki amejibu kwa hisia nzito, akieleza kusikitishwa na jinsi nia yake njema ilivyotafsiriwa vibaya mbele ya umma.

Hapa chini ni kauli yake kamili:

“Binadamu mbona tuna roho nyepesi kama korosho? 😢 Kwa nini mnanitengenezea taswira mbaya mbele ya hadhira yangu, ilhali nia yangu ilikuwa njema? Sitaki sifa wala umaarufu—nilitaka kusaidia kwa moyo wa huruma. Kumbukeni, kuna leo na kesho… na mitandao haitasahau kamwe. INTERNET NEVER FORGETS.”

“Kwa kuwa Nyevu Fondo hajaweza kupokea mchango huu, nimeamua pesa hizi nizielekeze kwenye kituo cha watoto yatima (Children’s Home) zikawe baraka kwa wengine. Labda Mungu ataniona na kunibariki. Kwa yote, nawaombea baraka – watu wa Mungu tuchukuliane kwa upendo.”

Awali Nyevu aliandika

Continue Reading

Entertainment

Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Published

on

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”

Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.

Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.

Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.

Continue Reading

Trending