Connect with us

News

Mpango wa Usambazaji Maji Kilifi Kuendelea

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano na serikali ya kitaifa kupitia Shirika la usambazaji umeme la REREC wanaendeleza mpango wa usambazaji umeme katika kaunti ya Kilifi.

Gavana wa kaunti hiyo, Gedion Mung’aro, amesema mpango huo unalenga kufikisha huduma za umeme mashinani ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kibiashara kwa urahisi.

Gavana Mung’aro amedokeza kwamba Shirika la REREC na kaunti ya Kilifi wamekuwa wakiwekeza kiwango flani cha fedha katika mpango huo ili kuhakikisha wakaazi wanapata huduma za umeme hadi mashinani.

Wakati huo huo amebainisha kwamba serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mradi wa usambazaji maji katika eneo bunge la Magarini katika juhudi za kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji eneo hilo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Chama cha DCP chashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha, 2025

Published

on

By

Uongozi wa chama cha DCP unashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025 ukidai una vipengee tata vitakavyoongeza mzigo wa ushuru kwa wakenya.

Kulingana na Naibu Kinara wa chama hicho Cleophas Malala, mswada huo hauzingatii hali ya uchumi ya wakenya ambao wanaendelea kukabiliana na gharama ya juu ya maisha.

Malala alitaja baadhi ya vipengee vinavyoibua maswali kama vile kodi mpya ya kuongezwa kwa ushuru wa VAT kwenye bidhaa za kawaida kama vile vyakula.

Akizungumza mjini Mombasa, Malala alishauri wakenya kuwa makini na kushiriki mchakato wa kuchambua mswada huo kikamilifu vile vile kutoa maoni kwa bunge kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.

Malala alimlaumu Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga pamoja na Rais William Ruto akidai wamezihadaa familia zilizowapoteza wapendwa wao mwaka jana wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha kwamba zingefidiwa.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Mamlaka ya KPA yalalamikia changamoto zinazolemaza shughuli zake.

Published

on

By

Licha ya Bandari ya Mombasa kuendelea kurekodi matokeo bora katika utendakazi wake,mamlaka ya bandari nchini (KPA) imebainisha kwamba bado kuna changamoto zinazolemaza shughuli zake.

Akizungumza katika kikao na kamati ya bunge kuhusu ushirikiano wa kikanda, mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kuwa changamoto hizo ni pamoja na idadi kubwa ya mashirika yanayokagua mizigo, vizuizi vya kupima uzito wa magari (weighbridges), na vizuizi vya polisi barabarani katika eneo la Kaskazini (Northern Corridor).

Kulingana na nahodha Ruto hali hiyo bado inaathiri ufanisi wa usafirishaji wa mizigo na biashara kwa ujumla.

Nahodha Ruto pia alieleza athari za ada zisizo rasmi zinazotozwa na mashirika mbalimbali, pamoja na ushuru wa CESS unaotozwa na serikali za kaunti kwa mizigo ambayo tayari imekaguliwa na kulipiwa bandarini.

Aliongeza kuwa gharama hizo za ziada zinaathiri ushindani wa Kenya kama kitovu cha biashara katika ukanda wa afrika mashariki.

Wakati uo huo, Ruto aliitaka serikali kuharakisha uboreshaji wa mifumo ya usafirishaji kwa kuongeza matumizi ya teknolojia na kuunganisha mifumo ya upimaji wa uzito wa magari kote nchini.

Kwa upande wake, kamati ya bunge kupitia kwa mwenyekiti wake, Bi. Irene Mayaka, iliahidi kwamba kamati hiyo itafuatilia kwa karibu malalamshi yaliyoibuliwa na kuhakikisha kwamba suluhu mwafaka inapatikana.

Taarifa ya mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending