Connect with us

Sports

Kikosi Cha Raga Morans Wamemaliza Ya Nne Mauritius

Published

on

Kikosi cha Raga wachezaji saba kila upande chipukizi Morans kimemaliza nafasi ya nne mashindano ya Bara la Afrika nchini Mauritius.

Hii ni baada ya vijana hao kupoteza fainali ya kusaka nafasi ya tatu kwa alama 21-19 dhidi ya Zimbabwe jana jioni.Mechi hiyo ilianza kwa moto vijana wa nyumbani wakichukua uongozi wa mapema 10-0 na badaye 12-0 ila Zimbabwe wakarejea kwa moto wa radi na kuzamisha matumaini ya vijana hao kumaliza tatu bora.

Vijana hao waliwazidi nguvu Nigeria alama 43-12 katika mechi ya robo fainali kabila ya kupoteza 14-12 dhidi ya Madagascar katika mechi ya nusu fainali.

Blitboks ya Afrika Kusini ndiyo waliibukia na ushindi wakitandika Madagascar alama 28-12 katika fainali iliopigwa Jumapili na sasa timu hizo mbili zinakwenda kuwakilisha Bara Afrika katika mashindano ya dunia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Fikirini Jacobs- Benni Mccarthy Ni Sahihi Harambee Stars

Published

on

By

Katibu katika Wizara Kuu ya Kitaifa Inayosimamia Maswala ya Vijana na Uchumi Bunifu Fikirini Jacobs amesifia hatua ya Shirikisho la soka nchini FKF na serikali kupitia kwa Wizara ya Michezo kumteua Benni Mccarthy kuwa kocha mkuu wa timu ya soka wanaume Harambee Stars.

Kwa mujibu wa Katibu huyo hatua hiyo ni ishara tosha ya kufufuka kwa mchezo huo nchini baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye timu hiyo.

“Nichukue Fursa Hii kuwapongeza Wizara ya Michezo ambapo yuko mwenzangu Elijah Mwangi sitaki nizungumz mengi lakini hata hatua ya Taifa La Kenya kumchukua Benni Mccarthy aliyekua kocha Manchester United kuwa kocha wa Harambee Stars ni hatua ya kufufua timu hiyo pamoja na The Lost Glory ,kwa sababu kihistoria mimi ni mtu nimekaa na watu wengi akiwemo mzee wetu The RT HON.Raila Amollo Odinga na aliwahi kuniambia hapa kenya mpira ulikua mkubwa mno kuliko magharibi na hata Afrika Kusini.”

Katibu huyo aliyasema hayo katika fainali ya mashindano ya kaunti ya shule za Upili katika shule ya Upili ya kilifi towship.

Continue Reading

Sports

Mchezaji Tenesi Alcaraz Bingwa Tena

Published

on

By

Mchezaji Tenesi anayeorodheshwa wa Pili duniani kwa sasa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ameweza kuandikisha rekodi mpya baada ya kushinda taji la pili kombe la Queens Cup Title baada ya kumlaza Jiri Licheka raia wa Czech kwa seti za 7-5, 6-7 (5/7), 6-2 kabila ya finali ya Wimblendon.

Nyota huyo raia wa Uhispania alimzidi mwenzake kwenye fainali baada ya kuonyesha makali tokea mwanzo huku mchezaji huyo anayeorodheshwa wa 30 akikubali kichapo hicho kwa muda lisali 2 na dakika 10.

Mwanatenesi huyo tayari ana mataji matano baada ya kuzishinda fainali za French Open,Rome Open,Monte Carlo na Rotherdam mwaka huu wa 2025.

Mwamba huyo hajapoteza katika mashindano fainali 18 mpaka sasa tangu fainali za Barcelona Open April 20.

Continue Reading

Trending