Connect with us

News

Miili iliyosalia Shakahola kuzikwa na Serikali

Published

on

Huenda serikali ikalazimika kuizika miili ya watu waliofariki dunia eneo la Shakahola, Magarini kaunti ya Kilifi baada ya zoezi la kuitambua miili hiyo kusitishwa.

Waziri wa usalama wa ndani, Kipchumba Murkomen alisema kuwa miili hiyo itazikwa katika sehemu moja na kisha sehemu hiyo kutengwa kama hifadhi ya kumbukumbu kwa waathiriwa.

Murkomen alisema kuwa zoezi hilo limekwama kutokana na familia nyingi kutojitokeza kuitambua miili hiyo akisema kuwa huenda ikawa miili mingi iliyopo kwa sasa sio ya watu waliokuwa wakaazi na wenyeji wa Kilifi.

“Hii miili sio ya Kilifi kaunti pekee bali Kenya nzima, Baringo, Vihiga, Siaya, Kisumu, maeneo hayo yote na sasa jamaa za watu hao hawajui kama watu waliopotea ni kweli walienda Shakahola na wakakufia huko, ndio maana hawajitokezi ili kufanyia sampuli za vinasaba”, alisema Murkomen

Kufuatia hilo Murkomen alihoji kuwa huenda serikali ikatumia njia mbadala kukamilisha zoezi hilo

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending