Connect with us

News

Migos: Serikali imeanzisha mipango ya kuimarisha idara ya ukaguzi wa shule

Published

on

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos Ogamba, alisema serikali imeanzisha mipango ya kuimarisha idara ya ukaguzi wa shule ili kuhakikisha fedha zinazotengewa taasisi za elimu zinatumika ipasavyo.

Akizungumza jijini Mombasa, Waziri Migos alieleza kwamba sekta ya elimu imetengewa mgao mkubwa katika bajeti ya kitaifa ya mwaka wa fedha wa 2025/2026 na kwamba ni lazima fedha hizo zitumike ipasavyo.

Waziri huyo vile vile alidokeza kwamba serikali inapanga kuajiri walimu elfu 24 katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha ujao ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu mashuleni.

“Kama serikali tumepanga kuajiri walimu wengine elfu 24 ili kukabiliana na changamoto za ukosefu wa walimu shuleni na kusaidia wanafunzi wetu kuendelea na masomo na pesa tumetenga ya kutosha”, alisema Migos.

Wakati uo huo, aliunga mkono uamuzi wa Mahakama kuu kupiga marufuku shule kutoza ada za ziada, akisema walimu wakuu wanaowatoza wazazi fedha zaidi kinyume na sheria, watakumbana na mkono wa sheria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending