Connect with us

News

Migos: Serikali imeanzisha mipango ya kuimarisha idara ya ukaguzi wa shule

Published

on

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos Ogamba, alisema serikali imeanzisha mipango ya kuimarisha idara ya ukaguzi wa shule ili kuhakikisha fedha zinazotengewa taasisi za elimu zinatumika ipasavyo.

Akizungumza jijini Mombasa, Waziri Migos alieleza kwamba sekta ya elimu imetengewa mgao mkubwa katika bajeti ya kitaifa ya mwaka wa fedha wa 2025/2026 na kwamba ni lazima fedha hizo zitumike ipasavyo.

Waziri huyo vile vile alidokeza kwamba serikali inapanga kuajiri walimu elfu 24 katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha ujao ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu mashuleni.

“Kama serikali tumepanga kuajiri walimu wengine elfu 24 ili kukabiliana na changamoto za ukosefu wa walimu shuleni na kusaidia wanafunzi wetu kuendelea na masomo na pesa tumetenga ya kutosha”, alisema Migos.

Wakati uo huo, aliunga mkono uamuzi wa Mahakama kuu kupiga marufuku shule kutoza ada za ziada, akisema walimu wakuu wanaowatoza wazazi fedha zaidi kinyume na sheria, watakumbana na mkono wa sheria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending