Connect with us

News

Migos, awataka walimu wakuu wa shule za upili kuwapa wanafunzi vyeti vya masomo

Published

on

Waziri wa Elimu nchini Julius Migos Ogamba amewataka walimu wakuu wa shule za upili kuwapa wanafunzi vyeti vyao vya masomo.

Ogamba vile vile aliwapongeza baadhi ya walimu waliowapa wanafunzi vyeti vyao vya mitihani ya kitaifa licha ya kuwa madeni ya Karo.

Ogamba alisema hatua za baadhi ya shule kutowakabidhi wanafunzi vyeti vyao vya mitihani ya Kitaifa ni kunyume cha sheria.

Akizungumza jijini Mombasa wakati wa kongamano la wakuu wa shule za upili, Ogamba alisema haipaswi kuwa hivyo kwani ni haki ya kila mwanafunzi kupokea cheti pindi tu anapokamilisha mtihani.

“Nachukua fursa hii kuwashukuru nyote hasa wale ambao mliwapa wanafunzi vyeti vyao licha ya wao kuwa na madeni ya karo, ila wakati niliwaambia kuhusu kupeana vyeti kwa wanafunzi hata kama wanadaiwa mlifanya vyema kwa sababu wakati ambapo unashikilia cheti hicho na hujalipwa pesa unazodai bado haina maana nyote mnateseka sababu wewe hujapata pesa unazodai na mwanafunzi pia hana cheti”. …alisema Ogamba.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending