Connect with us

News

Mhubiri mwenye utata Gilbert Deya ameaga dunia

Published

on

Mhubiri mwenye utata Gilbert Deya ameaga dunia baada ya kuhusika kwenye ajali ya barabarani katika eneo la Namba-Kapiyo kwenye barabara ya Bondo-Kisian maeneo ya Nyanza ajali ambayo imeacha watu wengine 30 na majeraha.

Kulingana na Kamanda wa trafiki eneo la Nyanza Peter Maina, ajali hiyo imehusisha magari matatu likiwemo gari la chuo kikuu cha Moi, gari la kaunti ya Siaya aina ya Toyota Fortuner na lengine Toyota Noah.

Maina alisema dereva wa gari aina ya Toyota Noah, lililokuwa likielekea eneo la Kisian sehemu za Bondo alipoteza mwelekeo na kugonga basi la chuo kikuu lililokuwa likielekea Kisumu.

Aidha alidokeza kwamba mhubiri Deya alikuwa akiendesha gari hilo aina ya Toyota Noah na alikuwa amebeba abiria wawili Wanawake mmoja akiaminika kuwa mkewe ambao wamepata majeraha madogo.

Wanafunzi 15 waliokuwa kwenye basi la chuo kikuu wamepata majeraha mabaya na wengine 15 wakapata majeraha madogo.

Mwili wa Deya ulichukuliwa na kuhifadhiwa katika makafani ya hospitali ya kaunti ndogo ya Kombewa huku baadhi ya majeruhi wakitibiwa katika hospitali hiyo na wengine katika hospitali ya rufaa ya Jaramogi Oginga Odinga.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending