Connect with us

News

Mhubiri mwenye utata Gilbert Deya ameaga dunia

Published

on

Mhubiri mwenye utata Gilbert Deya ameaga dunia baada ya kuhusika kwenye ajali ya barabarani katika eneo la Namba-Kapiyo kwenye barabara ya Bondo-Kisian maeneo ya Nyanza ajali ambayo imeacha watu wengine 30 na majeraha.

Kulingana na Kamanda wa trafiki eneo la Nyanza Peter Maina, ajali hiyo imehusisha magari matatu likiwemo gari la chuo kikuu cha Moi, gari la kaunti ya Siaya aina ya Toyota Fortuner na lengine Toyota Noah.

Maina alisema dereva wa gari aina ya Toyota Noah, lililokuwa likielekea eneo la Kisian sehemu za Bondo alipoteza mwelekeo na kugonga basi la chuo kikuu lililokuwa likielekea Kisumu.

Aidha alidokeza kwamba mhubiri Deya alikuwa akiendesha gari hilo aina ya Toyota Noah na alikuwa amebeba abiria wawili Wanawake mmoja akiaminika kuwa mkewe ambao wamepata majeraha madogo.

Wanafunzi 15 waliokuwa kwenye basi la chuo kikuu wamepata majeraha mabaya na wengine 15 wakapata majeraha madogo.

Mwili wa Deya ulichukuliwa na kuhifadhiwa katika makafani ya hospitali ya kaunti ndogo ya Kombewa huku baadhi ya majeruhi wakitibiwa katika hospitali hiyo na wengine katika hospitali ya rufaa ya Jaramogi Oginga Odinga.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending