Business
Mgomo wa Tuktuk Tezo waathiri biashara

Shughuli za kibiashara katika soko la Tezo kaunti ya kilifi ziliathirika jumatatu ya Julai, 21, 2025 kufuatia mgomo wa wahudumu wa tuktuk.
Kulingana na wafanyibiashara katika soko hilo, wengi wao wanategemea huduma za tuktuk kusafirisha bidhaa zao hadi katika soko hilo.
Wakizungumza na cocofm wafanyibiashara hao waliongeza kuwa wateja wengi pia hutegemea usafiri wa tuktuk kufika sokoni humo, na kufuatia mgomo huo wengi walikosa kufika hali ambayo iliwasababishia hasara kubwa.
Aidha waliitaka sekta ya tuktuk kurejesha huduma hizo ili kuwapa afueni wafanyibiashara ikizingatiwa kuwa wanategemea biashara kujikimu kimaisha.
Mgomo huo wa wahudumu wa tuktuk uliwapa wadumu wa bodaboda mjini kilifi kaunti ya kilifi fursa ya kuvuna zaidi kimapato.
Kulingana na wanaboda wa eneo la Tezo mgomo wa wahudumu wa tuktuk uliwapelekea fursa ya kuongeza nauli kutokana na idadi kubwa ya wateja.
Kutoka eneo la Tezo hadi Chumani wahudumu hao walibeba abiria mmoja kwa shilingi 200 tofauti na shilingi 100 ya hapo awali.
Wahudumu wa tuktuk waligoma kutokana na kupanda kwa bei za mafuta aina ya petroli na dizeli, hali ambayo wanasema inasawababishia harasa kubwa.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Mradi wa kiuchumi wa Dongo Kundu wavutia wawekezaji zaidi

Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaendelea kuonyesha nia ya kuekeza katika mradi wa kiuchumi wa dongo kundu kaunti ya Mombasa.
Mradi huo unaotarajiwa kuongeza uzalishaji katika viwanda na thamani ya bidhaa ndani ya nchi na nje, unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Kampuni ya nishati kutoka China, Ruike Energy Group Limited, ni mwekezaji wa hivi karibuni kuonyesha nia ya kupata nafasi ndani ya eneo hilo la kiuchumi la Dongo Kundu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta.
Kulingana na halmashauri ya bandari nchini KPA hatua hiyo italeta faida Zaidi ikiwemo kubuni nafasi za ajira, ikuaji wa uchumi, upatikanaji wa vifaa vya baharini, na urahisi wa kufikia masoko ya kanda na ya kimataifa.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
KETRACO kuimarisha usalama wa chakula nchini

Shirika la usambazaji umeme nchini, KETRACO, limethibitisha dhamira yake ya kuimarisha usalama wa chakula, ukuaji wa kijani, na ushirikiano wa kieneo kupitia uekezaji mkubwa katika miundombinu ya umeme.
Katika maonesho ya Kimataifa ya kilimo ASK yanayoendelea kaunti ya Mombasa, KETRACO imeonyesha jinsi miundombinu yake ya umeme inavyowezesha kilimo cha kisasa na uzalishaji wa viwandani.
Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi mkuu, mhandisi Kipkemoi Kibias, KETRACO imekamilisha miradi 43 ya njia za kusafirisha umeme, huku mingine 29 ikitarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2028.
Kibias, alisema shirika hilo tayari limejenga zaidi ya kilomita elfu sita za njia za umeme wa msongo mkubwa, likiwa pia na vituo 46 vya kusambaza umeme na upanuzi wa mitambo 33.
Katika eneo la Pwani, Kibias alisema upanuzi wa mpango wa Green Energy Backbone umewezesha usambazaji wa kawi safi kwa asilimia 93, jambo lililopunguza utegemezi wa mafuta na kuchochea maendeleo ya biashara za kilimo, utalii na uchumi wa baharini.
Kibias alisema KETRACO inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuunganisha Kenya na nchi jirani kupitia njia za kimataifa kama zile za Ethiopia, Tanzania na Uganda hatua zitakazowezesha biashara ya umeme Afrika Mashariki.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
-
News18 hours ago
Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi
-
Sports17 hours ago
Kocha wa Uingereza Thomas Tuchel akataa madai ya “laana” huku akilenga kuvunja ukame wa miaka 60 wa mataji makubwa
-
Sports17 hours ago
Lionel Messi afunga mabao mawili akiiongoza Argentina, huku Uruguay, Colombia na Paraguay wakifuzu Kombe la Dunia 2026