Connect with us

News

Mbunge wa Kilifi kaszkazini Owen Baya alaumiwa na wanaharakati.

Published

on

Wanaharakati wa kupambana na utumizi wa dawa za kulevya kanda ya pwani wamemkosoa mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya kutokana na hatua ya kuondoa hoja bungeni ya kupinga biashara ya zao la Mugoka.

Wakiongozwa na Famau Mohammed Famau, wanaharakati hao walisema uraibu wa mugoka umeendelea kuathiri maisha ya vijana wengi pwani na walikuwa na matumaini na mbunge huyo kukomboa maisha ya vijana kupitia hoja hiyo.

Famau alimshauri Baya kutowasilisha barua rasmi ya kuhakiki kuondoa hoja hiyo bungeni, ila kuendelea na harakati za kupambana na uraibu wa mugoka na kukomboa maisha ya vijana wa pwani.

“Mheshimiwa Baya alipochukuwa mswada huu kuupeleka bungeni sisi tulifurahi sana na kumpongeza, na hivi sasa kuuondosha bungeni tumekasirika na amefanya jambo la aibu ambalo halingefaa kufanywa na kiongozi kama yeye”, alisema Famau.

Kwa upande wake afisa mratibu mipango katika shirika la Kenya Muslim Youth alliance Asili Randani, aliitaka serikali kuu kuhusisha vijana katika miradi inayoendelea ili kuwaepusha na uhaba wa ajira unaoshuhudiwa miongoni mwao.

“Hapa eneo bunge la Kilifi kaskazini kunajanga kubwa la matumizi ya dawa za kulevya, miradi hii ingehusisha jamii moja kwa moja vijana wetu wasinge kuwa katika swala lile, vijana wakula mugoka wengi wao wamepoteza mwelekeo na wamekuwa wazembe”, alisema Randani.

Afisa mratibu mipango katika shirika la Kenya Muslim Youth alliance Asili Randani akizungumza na wanahabari Kilifi

Itakumbukwa mapema mwaka jana wa 2024 baadhi ya magavana eneo la pwani walipiga marufuku biashara ya zao la mugoka japo vita hivyo havikufaulu.

Taarifa ya Joseph Jira.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Published

on

By

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.

Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.

Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.

Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.

Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending