News
Mboko: Uongozi wa Rais Ruto haujawabagua wapwani

Mbunge wa Likoni Mishi Mboko amempongeza rais William Samoei Ruto, akisema uongozi wake haujawabagua wakaazi wa Pwani katika masuala ya maendeleo.
Akizungumza mjini Garsen katika kaunti ya Tana River, wakati wa ziara ya Naibu wa Rais Prof. Kithure Kindiki katika kaunti hiyo, Mishi alisema wataendelea kushirikiana na rais Ruto ili Pwani inufaike kimaendeleo.
Mishi pia aliwasihi viongozi na wakaazi wa Pwani kushirikiana na Rais Ruto ili kuiboresha Pwani kimaendeleo na taifa la Kenya kwa jumla.
Mishi alisema Rais Ruto ana malengo mengi na mazuri kwa taifa la Kenya na amekuwa pia akiendeleza juhudi za kuwaunganisha Wakenya ili waishi kwa umoja.
“Nasi tunasema kufa kufaana tutakufa na Daktari William Ruto, kuzama na kuzuka’’, alisema Mishi.
Mishi pia alisema utawala wa rais Ruto haujawabagua dini ya kiislamu katiwaumekuwa ikishirikisha jamii ya waislamu katika masuala mbalimbali.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.
Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.
Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.
“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.
Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.
Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.
Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.
Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.
Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.
Taarifa ya Mwanahabari wetu