Connect with us

News

Mboko: Dhulma za kijinsia dhidi ya watoto lazima zikomeshwe

Published

on

Mbunge wa Likoni Bi Mishi Mboko amewakosoa baadhi ya wakaazi wa eneo bunge hilo kwa madai ya kukosa kuchukulia kwa uzito kesi za dhulma za kijinsia dhidi ya watoto.

Bi Mboko alisema vitendo hivyo vinakiuka haki za mtoto na wenyeji wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanadhibiti visa hivyo.

Bi Mboko ambaye alikuwa akizungumza katika eneo bunge lake la Likoni, alisema kuna haja ya wakaazi kuripoti visa hivyo kwa asasi za kiuslama ili washukiwa wa visa hivyo wakabiliwe kisheria.

“Hizi kesi za Femicide na GBV kwa nini ushahidi upotee polisi, ati evidence hakuna na mtoto ameletwa akiwa yuko katika zile hali na kila kitu alafu ati ushahidi unapotea, please handle these cases with the heart of humanity’’, alisema Bi Mboko.

Vilevile, aliwahimiza maafisa wa polisi kuwajibika vilivyo pindi kesi hizo zinaporipotiwa kwao.

Wakati huo huo, alitoa wito kwa wenyeji wa Likoni kushirikiana na vitengo vya usalama ili kudhibiti visa vya watoto wenye umri mdogo kujiungiza katika uhalifu na kuhakikisha watoto hao wanapelekwa katika vituo vya kurekebisha tabia.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Waislam Waadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha

Published

on

By

Waislam kote duniani wanaadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha, inayojulikana pia kama sikukuu ya sadaka, ambayo huadhimishwa katika mwezi wa Dhul Hijjah katika kalenda ya Kiislam.

Sikukuu hii ni moja ya nyakati tukufu zaidi katika Uislamu, ikiashiria kilele cha Hijja na kuadhimisha utiifu wa Nabii Ibrahimu aliyekuwa tayari kumtoa mwanawe Ismail kama sadaka kwa amri ya Mwenyezi Mungu.

Siku kumi za mwanzo za Dhul Hijjah zinahesabiwa kuwa siku takatifu zaidi, zikiwa zimejawa na ibada, kufunga, na dua.

Mwaka huu, zaidi ya mahujaji milioni 2 wanahudhuria Hijja katika mji mtakatifu wa Makkah nchini Saudi Arabia, Kenya ikipeleka wahujaji 4,500, kuhijji, ikiwa ni mojawapo ya idadi kubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni.

Viongozi mbalimbali wa dini ya kiislam waliwahimiza waumini wa dini ya kiislam kuhakikisha wanasheherekea sikukuu ya Eid-ul-Adha pamoja na wale wasiojiweza kwa kuchinja mifugo na kugawa na watu wengine wasiobahati katika jamii.

Taarifa ya Lolani Kalu

Continue Reading

News

Familia zilizoathirika na ujenzi wa barabara kuu ya Kilifi-Mtwapa zafidiwa.

Published

on

By

Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imesema serikali inaendelea na zoezi la kufidia familia zilizoathirika na ujenzi wa barabara kuu ya Kilifi kuelekea Mtwapa.

Kamisha wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alidokeza kuwa kwa sasa maafisa wa shirika la Kenya power wanaendelea kuondoa nyaya za stima ili kutoa nafasi kwa mkandarasi kuendelea na shughuli za ujenzi.

Vile vile Biwot alisema ujenzi daraja mbili kubwa kaunti ya Kilifi unaendelea pamoja na ujenzi wa barabara ya Sabaki Sosoni kueleke Baricho hadi Baolala.

“Ujenzi wa barabara kuu ya Kilifi kuelekea Mtwapa unaendelea vyema, tunachokifanya sasa ni kufidia walioathirika, pia kenya power inaondoa nyaya kupisha mwanakandarasi kuendelea na ujenzi, vile vile ujenzi wa daraja mbili kuu kilifi unaendelea hasa ya Galana Kulalu na Baricho”, alisema Biwot.

Vile vile Kamishna huyo alidokeza kuwa serikali inaendelea na ujenzi wa miradi mbali mbali inayoambatanishwa na sekta ya uchumi wa bahari.

“Upande wa uchumi wa bahari miradi mingi inaendelea mfano ujenzi wa eneo la kuegesha boti kilifi, pia tunajenga makao makuu ya eneo la samaki ya kaunti, tuko na soko la samaki Malindi, tuko na eneo la kuhifadhi samaki la kichwa cha kati ambalo limekamilika na liligharimu shilingi milioni 250”, aliongeza Biwot.

Wakati huo huo wadau wa sekta ya Uvuvi eneo la Ngomeni wakiongozwa na Mwenyekiti wa Ngomeni BMU Said Athman aliitaka serikali kufuatilia kwa kina fedha zinazotolewa na serikali kudaidi miradi ya wavuvi.

“Tunapewa pesa ya makundi kwa mfano shilingi milioni tatu, ile pesa mpaka ikifikia jamii imeliwa, kwa mfano unapewa boti lakini halina vifaa sababu ile pesa imeliwa juu na maofisa mpaka ikifika nyanjani imeisha”, alisema Athman.

Mwenyekiti wa Ngomeni BMU Said Athman akizungumza na wanahabari Kilifi.

Taarifa ya Joseph Jira.

 

 

Continue Reading

Trending