Connect with us

News

Mboko: Dhulma za kijinsia dhidi ya watoto lazima zikomeshwe

Published

on

Mbunge wa Likoni Bi Mishi Mboko amewakosoa baadhi ya wakaazi wa eneo bunge hilo kwa madai ya kukosa kuchukulia kwa uzito kesi za dhulma za kijinsia dhidi ya watoto.

Bi Mboko alisema vitendo hivyo vinakiuka haki za mtoto na wenyeji wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanadhibiti visa hivyo.

Bi Mboko ambaye alikuwa akizungumza katika eneo bunge lake la Likoni, alisema kuna haja ya wakaazi kuripoti visa hivyo kwa asasi za kiuslama ili washukiwa wa visa hivyo wakabiliwe kisheria.

“Hizi kesi za Femicide na GBV kwa nini ushahidi upotee polisi, ati evidence hakuna na mtoto ameletwa akiwa yuko katika zile hali na kila kitu alafu ati ushahidi unapotea, please handle these cases with the heart of humanity’’, alisema Bi Mboko.

Vilevile, aliwahimiza maafisa wa polisi kuwajibika vilivyo pindi kesi hizo zinaporipotiwa kwao.

Wakati huo huo, alitoa wito kwa wenyeji wa Likoni kushirikiana na vitengo vya usalama ili kudhibiti visa vya watoto wenye umri mdogo kujiungiza katika uhalifu na kuhakikisha watoto hao wanapelekwa katika vituo vya kurekebisha tabia.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mawakili Kilifi waungana kushtumu mauaji ya Wakili Mbobu

Published

on

By

Siku chache baada ya Wakili Kyalo Mbobu kuuawa kinyama kwa kupigwa risasi mara kadhaa akiwa kwenye gari lake barabara ya Lang’ata jijini Nairobi, mawakili mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wameungana na mawakili wengine nchini siku ya Ijumaa Semtemba 12 mwaka huu kufanya matembezi ya amani, wakishutumu vikali mauaji hayo.

Wakiongozwa na Mwakilishi wao Sesil Mila, mawakili hao walilaani vikali mauaji ya wakili Mbobu wakiishutumu serikali kwa kutowajibikia swala la usalama wa wananchi wake.

Aidha waliitaka idara ya usalama kuhakikisha kuwa inafanikisha wajibu wake wa kuwalinda mawakili wakisisitiza haja ya haki kupatikana kwa familia ya mwendazake wakili Kyalo.

Mawakili wa Kilifi wakiongozwa na Sesil Mila, washtumu mauaji ya Wakili Kyalo Mbobu

Mawakili hao sasa waliitaka idara ya upelezi na asasi zote husika kuhakikisha kuwa uchunguzi wa kina unafanywa kubaini watuhumiwa wa mauaji hayo ili wachukuliwe hatua kali za kisheria haraka iwezekanavyo.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

IEBC inaendelea kutambua vituo vya kusajili wapiga kura

Published

on

By

Maafisa wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wamesema wanaendelea na zoezi la kutambua sehemu za kuweka vituo vya kusajili wapiga kura hasa maeneo ya mashinani.

Afisa msimamizi wa tume ya IEBC eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Mohammed Bahero Aboud alisema juhudi hizo ni kuhakikisha zoezi la usajili wapiga kura litakaloanza rasmi Septemba 29, mwaka huu linafaulu.

Akizungumza mjini Kilifi, Bahero alisema tume hiyo inatumia mbinu mpya ya kutambua vituo vya jadi vya usajili wapiga kura na kuweka vituo vipya kulingana na mapendekezo ya sheria.

Wakati huo huo alidokeza kwamba tume ya IEBC imekuwa ikihamashisha wakenya kutokubali kushawishiwa na wanasiasa na kujisajili katika maeneo yasiokuwa yao hasa msimu huu ambao zoezi hilo linakaribia kuanza.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending