Connect with us

Entertainment

Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa

Published

on

Mwanamuziki mashuhuri wa Congo (DRC) Mbila Bel, anaendelea kupata matibabu katika Hospitali Moja Mjini Kinshasa, baada ya Gari alimokuwa akisafiria kuhusika kwenye ajali ya barabarani Septemba 9.

Kwa mujibu wa taarifa za vyanzo vya habari mjini Kinshasa, Mama Mbila Bel alikuwa safarini kuelekea uwanja wa Ndege wa N’djili, ili kuabiri Ndege akiwa na meneja wake wa muziki Jules Nsana ambaye pia alijeruhika

Mbila Bel ambaye jina lake halisi ni Marie Claire Mboyo, alitarajiwa kusafiri kuelekea nchini Ubelgiji kuwatumbuiza mashabiki wake katika ukumbi wa Madeleine Jijini Brussels, wakati ajali hiyo ilipotokea, baada ya dereva wake kushindwa kulithibiti gari lao.

Hali yake ya kiafya inatajwa kuwa mbaya na anahitaji Kwa dharura huduma za upasuaji na kina mipango ya kumhamishia Hospitali nyingine kwa matibabu zaidi.

Mbila Bel alizaliwa January 10 1959 na kupindukia kuwa maarufu kimuziki kunako miaka ya 70 alipojiunga na bendi ya Afrisa international ikiongozwa na Pascal Tabu Ley Rochereau.

Miongoni mwa nyimbo zake zilizotoa fora ni pamoja na Eswi Yo Wapi, Tempelo, Mpeve Ua Longo, Faux Pas, Beyanga, Yamba Ngai, Nairobi and Nadina.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake

Published

on

Mmiliki wa Crack Sound Records, J Crack, amepata pigo kubwa baada ya studio yake kuvamiwa na wezi walioiba vyombo vyake vya studio.

Akizungumza na kipindi cha Coco Drive cha COCO FM, msanii huyo alieleza kwa masikitiko jinsi wezi walivyoiba kila kitu, kuanzia vifaa vya muziki hadi mali ndogo ndogo za studio.

“Wameiba hadi kufuli ya mlango, computer ya kazi niliyotoka nayo Ulaya, laptop, TV mbili za reception na studio, electric guitar, piano… CCTV nimenunua sasa baada ya kuibiwa,” alisema J Crack kwa majonzi.

Kisa hiki kimewavunja moyo wasanii waliokuwa wakifanya kazi chini ya lebo hiyo, ikiwemo Susumila, ambaye pia alikuwa na mradi wake binafsi studioni humo.

J Crack pia alidokeza kwamba alikuwa akipanga kuachia EP mpya, lakini sasa mipango hiyo imelazimika kusimama kwa muda kufuatia hifadhi ya EP yake kuibwa pamoja na vyombo vyake.

Licha ya kupoteza mali nyingi, J Crack anasema hana mpango wa kukata tamaa.

“Mwizi hajanikata miguu. Crack Sound siyo mashine, ni vichwa. Wangenikata kichwa hapo sasa wangekuwa wamenimaliza. Tunaendelea mbele,” alisisitiza.

J Crack pia alisema kwamba Susumila ambaye alipata taarifa hizo aliahidi kumsaidia kuwapata walihusika kutekeleza wizi huo akisema kwamba atayashughulikia kinyumbani.

“Susumila aliniambie tumuachie yeye, halafu sisi tudeal na polisi,” alisema kwa msisitizo.

Mashabiki wa muziki wameeleza masikitiko yao mtandaoni, wakimtakia J Crack na timu yake nguvu mpya na kurejea kwa kasi kwenye game.

Continue Reading

Entertainment

Paula Kajala Afunguka Sababu ya Kumtema Rayvanny

Published

on

Mwanamitindo na mtangazaji maarufu kutoka Tanzania, Paula Kajala, hatimaye amevunja ukimya na kueleza sababu za kuachana na msanii nyota Rayvanny.

Katika mahojiano ya wazi, Paula alifichua kuwa uhusiano huo haukuweza kudumu kwa sababu ya kile alichokitaja kama kukosa uthabiti na kutoheshimu hisia za wanawake kwa upande wa msanii huyo.

Paula alisema kuwa safari yake ya mapenzi na Rayvanny ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

“Hajali hisia za mtu yeyote. Alikuwa na Fahima, akaja kwangu, baadaye akaonekana na Feza, na sasa amerudi tena kwa Fahima. Hivyo basi, msishangae kesho mkimuona na mwanamke mwingine. Kwake yeye ni kiki na kubaki trending tu,” Paula alieleza.

Kulingana naye, mabadiliko ya mara kwa mara ya msanii huyo kati ya wanawake mbalimbali yalifanya iwe vigumu kujenga mustakabali thabiti wa pamoja.

Paula alitumia nafasi hiyo kuonya wanawake wanaotamani kuwa na uhusiano na watu mashuhuri kama Rayvanny kuchukua tahadhari.

“Wanawake wanapaswa kuchunguza tabia ya mwanaume kabla ya kuingia kwenye uhusiano. Kwa Rayvanny, mara nyingi huwa ana wanawake kadhaa kwa wakati mmoja,” aliongeza.

Kauli za Paula zilisambaa kwa kasi mitandaoni, zikizua mjadala mpana kuhusu changamoto za kuwa na uhusiano na wasanii wakubwa.

Wengi walihoji kama maisha ya umaarufu yanaweza kuendana na mahusiano ya kudumu, huku wengine wakiona kuwa tabia ya Rayvanny ni taswira ya changamoto zinazowakabili wanawake wengi wanaojaribu kujenga familia na wanaume maarufu.

What do youy think?

Continue Reading

Trending