Sports
Mbeumo United Ndiyo Chaguo Langu

Kiungo mshamabulizi wa kilabu ya Brenford na Cameroon Bryan Mbeumo ameweka wazi kuwa anapendelea kujiunga na kilabu ya Manchester United pekee msimu huu.
Mchezaji huyo ambaye alifunga magoli 20 msimu uliopita anasema hatakubali ofa kwiengineko iwapo united hawataendelea na dili hio kumpeleka Old Trafford.
Kilabu ya Manchester United wanatarajiwa kuwasilisha ofa ya pili kusaka hudumza za winga huyo,
Hii ni baada ya ofa ya kwanza ya pauni milioni 55 kukataliwa na Brenford wiki moja iliopita.
Brenford wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo nyota ambaye pia anamezewa mate na kilabu ya Tottenham Ya Uingereza.
Sports
Fikirini Jacobs- Benni Mccarthy Ni Sahihi Harambee Stars

Katibu katika Wizara Kuu ya Kitaifa Inayosimamia Maswala ya Vijana na Uchumi Bunifu Fikirini Jacobs amesifia hatua ya Shirikisho la soka nchini FKF na serikali kupitia kwa Wizara ya Michezo kumteua Benni Mccarthy kuwa kocha mkuu wa timu ya soka wanaume Harambee Stars.
Kwa mujibu wa Katibu huyo hatua hiyo ni ishara tosha ya kufufuka kwa mchezo huo nchini baada ya ukimya wa muda mrefu kwenye timu hiyo.
“Nichukue Fursa Hii kuwapongeza Wizara ya Michezo ambapo yuko mwenzangu Elijah Mwangi sitaki nizungumz mengi lakini hata hatua ya Taifa La Kenya kumchukua Benni Mccarthy aliyekua kocha Manchester United kuwa kocha wa Harambee Stars ni hatua ya kufufua timu hiyo pamoja na The Lost Glory ,kwa sababu kihistoria mimi ni mtu nimekaa na watu wengi akiwemo mzee wetu The RT HON.Raila Amollo Odinga na aliwahi kuniambia hapa kenya mpira ulikua mkubwa mno kuliko magharibi na hata Afrika Kusini.”
Katibu huyo aliyasema hayo katika fainali ya mashindano ya kaunti ya shule za Upili katika shule ya Upili ya kilifi towship.
Sports
Mchezaji Tenesi Alcaraz Bingwa Tena

Mchezaji Tenesi anayeorodheshwa wa Pili duniani kwa sasa Carlos Alcaraz raia wa Uhispania ameweza kuandikisha rekodi mpya baada ya kushinda taji la pili kombe la Queens Cup Title baada ya kumlaza Jiri Licheka raia wa Czech kwa seti za 7-5, 6-7 (5/7), 6-2 kabila ya finali ya Wimblendon.
Nyota huyo raia wa Uhispania alimzidi mwenzake kwenye fainali baada ya kuonyesha makali tokea mwanzo huku mchezaji huyo anayeorodheshwa wa 30 akikubali kichapo hicho kwa muda lisali 2 na dakika 10.
Mwanatenesi huyo tayari ana mataji matano baada ya kuzishinda fainali za French Open,Rome Open,Monte Carlo na Rotherdam mwaka huu wa 2025.
Mwamba huyo hajapoteza katika mashindano fainali 18 mpaka sasa tangu fainali za Barcelona Open April 20.