Connect with us

International News

Matumaini ya kusitisha vita Gaza yaanza

Published

on

Licha ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kwamba mpango wa usitishaji mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa Gaza unakaribia, kundi la Hamas limeeleza kwamba bado mazungumzo yanaendelea.

Katika kile kinachoonekana kama jibu la kwanza la Hamas tangu Rais Trump kutangaza kupatikana kwa mwafaka huo, kundi hilo lilisema kwamba bado linaendelea kuyatafakari mapendekezo mapya yaliyomo kwenye mpango huo.

“Tunalichukulia suala hili kwa uangalifu mkubwa. Tunafanya majadiliano ya kitaifa kuyatathmini mapendekezo ya ndugu zetu wapatanishi”, lilisema kundi hilo kupitia Kiongozi wao.

Mnamo siku ya Jumanne Julai mosi mwaka huu, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Israel ilikuwa imekubaliana na masharti ya kusitisha mapigano kwa siku 60 wakati mauaji kwenye ukanda wa Gaza yakiwa kwenye mwezi wake wa 21.

Trump alidai kwamba Misri na Qatar, ambazo ni wapatanishi wakuu, walikabidhiwa jukumu la kuwafikishia mapendekezo hayo Hamas lakini wakati huo huo akilitishia kundi hilo kutokuutakaa mpango huo.

“Tunaamini kwamba Misri na Qatar wanaendelea na mpango mzuri wa upatanisho na suala hili linafaa kuchukuliwa kwa uzito zaidi lakini pia ni lazma Hamas iwe waangalifu na kuzingatia masharti hayo”, alisema Trump.

Baraza la usalama lajadili upatishi Gaza.

Waziri wa Mambo ya nje wa Israel, Gideon Saar, alisema sehemu kubwa ya mawaziri kwenye serikali ya nchi yake wanaunga mkono makubaliano hayo ambayo yanajumuisha kuachiliwa kwa mateka.

Waziri huyo wa mambo ya kigeni aliongeza kwamba sehemu kubwa ya raia wa Israel wanaunga mkono makubaliano hayo kama inavyothibitishwa na uchunguzi wa maoni.

Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatarajiwa kukutana na Rais Trump wiki ijayo mjini Washington, ili kuangazia zaidi mikakati na mipango ya kudhibiti.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni

Published

on

By

Mahakama kuu nchini Tanzania imemrejesha kwenye debe mgombea urais wa chama cha upinzani ACT wazalendo, Luhaga Mpina na kupindua maamuzi yaliyotolewa na tume ya uchaguzi nchini humo INEC.

Hii inamaana tume ya INEC ni lazima imjumuishe Mpina katika orodha ya majina ya watakaopigiwa kura, hatua itakayosababisha upinzani kwenye uchaguzi huo mkuu.

Hatua hii sasa inampa Mpina fursa ya kuanzisha kampeni za kutaka kumbandua mamlakani rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29 mwaka 2025.

Kampeni za uchaguzi tayari zinaendelea nchini humo.

INEC ilimzuia mpina kugombe wadhifa wa urais mwezi Agosti 26, 2025 ikidai chama cha ACT Wazalendo kilikiuka taratibu za chama kwa kumsimamisha Mpina kuwania wadhifa huo.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa katika kampeni za uchaguzi mkuu.

Katika uamuzi uliotolewa Alhamisi  mwezi Septemba 11, 2025, jopo la majaji watatu mjini Dodoma liliagiza INEC kumuidhinisha Mpina kama mgombea wa urais.

Anatarajiwa kujumuika na wagombea wengine 16 kutoka vyama vidogo vya kisiasa katika mapambano hayo ya kuwania urais, ambao wote wanania ya kung’atua rais wa sasa Samia Suluhu Hassan mamlakani.

Chama cha Chadema kilizuiwa kugombea katika uchaguzi huo baada ya kiongozi wake Tundu Lissu kufunguliwa mashtaka ya uhaini.

Kiongozi wa upinzani wa Chadema Tundu Lissu akiwa mahakamani.

Rais Samia Suluhu Hassan alichukua hatamu za uongozi kama rais baada ya kifo cha John Pombe Magufuli mwaka 2021.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

International News

Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Published

on

By

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.

Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.

Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.

Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.

Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

Trending