Connect with us

Sports

Mashemeji Debi ni Jumapili

Published

on

Mwenyekiti wa maandalizi ya CHAN mwezi Agosti nchini Nicholas Musonye amezionya vikali mashabiki wa Afc Leopards na Gor Mahia dhidi ya vurugu ya aina yoyote siku ya Jumapili Debi la Mashemeji. Kwenye kikao na wanahabari Musonye amesema iwapo viti vitangolewa au mawe kurushwa au rabsha ya aina yoyote basi vilabu hivyo vitakua hatarini.

“Viwanja vya Nyayo na Kasarani vimekarabatiwa rasmi kwa ajili ya michuano ya CHAN natoa onyo kwa mashabiki wa Afc na Gor iwapo viti vitangolewa ama Mawe kurushwa au rabsha ya aina yoyote hawatumia Tena viwanja hivi na watapata adabu Kali mno.

Vilabu hivyo viwili vinakutana kwa mara ya kwanza msimu huu mechi ya pili ikipigwa April 14 . Afc Leopards ndio wenyeji wa mechi hiyo na tayari tiketi zimeanza kuuzwa shilingi 500 mashabiki wa kawaida na 1000 mashabiki mashuhuri.Gor Mahia wako nafasi ya tatu ligini na alama 45 wakati Afc Leopards wakiwa ya Tano alama 39.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Taifa Ya Nigeria Super Falcons Imepokea Zawadi Nono Kutoka Kwa Rais

Published

on

By

 Mabingwa wa Bara Afrika kwa soka la akina dada Super Falcons wamevuna vinono kutoka kwa rais wa taifa hilo punde tu baada ya kutua kutoka mjini Rabat Morocco.
Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu akitangaza zawadi zifuatazo kwa timu ya Super Falcons:
Kila mchezaji atapokea dola 100,000 za Kimarekani
Kila mchezaji atapewa nyumba ya vyumba vitatu
Kila mwanachama wa benchi la ufundi atapokea dola 50,000 za Kimarekani
Zaidi ya hayo, Jukwaa la Magavana wa Nigeria limewazawadia kila mchezaji kiasi cha ₦10 milioni (takriban dola 6,000 za Kimarekani).
Vipusa hao waliwashinda wenzao wa Morocco magoli 3-2 kwenye fainali kali iliosakatwa siku ya Jumamosi na kutwa ubingwa huo likiwa ni taji lao la kumi katika historia ya kombe hilo.
Continue Reading

Sports

Morocco Waanza Mazoezi Nyayo Tayari Kwa CHAN

Published

on

By

SIKU 4 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN
Timu ya Taifa Ya Morocco marufu ‘Atlas Lions ‘ wamefanya mazoezi Yao ya kwanza Ugani Nyayo hapo jana kujinoa tayari kwa mechi ya ufunguzi.
Vijana hao waliwasili mapema Jana tayari kwa kipute hicho kinachongoa nanga Jumamosi hii ugani Benjamin Mkapa nchini Tanzania.
Badhi ya wachezaji nyota kwenye kikosi hicho ni pamoja na;mshambulizi El Mahraoui Anas pamoja na kiungo Khairi Ayoub wa RS Berkane.
Hii hapa ni kikosi chote cha Taifa hilo kwa kombe la CHAN;
Magolikipa:
  • Al Harrar Elmehdi
  • Rachid Ghanimi (FUS Rabat)
  • Aqzdaou Omar (Wydad Casablanca)

Mabeki:

  • Moufid Mohamed (Wydad Casablanca)
  • Boulacsout Mohamed
  • Mchakhchekh Mehdi
  • Louadni Marouane
  • Arrassi Bouchaib
  • Assal Abdelhak (RS Berkane)
  • Belammari Youssef (Raja Casablanca)
  • Zahouani Fouad

Viungo:

  • Khairi Ayoub (RS Berkane)
  • Hrimat Mohamed Rabie
  • Souane Amine
  • Essadak Houssam
  • Hajji Reda (RS Berkane)
  • Bach Anas
  • Aït Ouarkhane Khalid
  • Bougrine Sabir

Washambulizi:

  • Mehri Youssef (RS Berkane)
  • El Mahraoui Anass
  • Bouhra Saïf-Eddine (Wydad Casablanca)
  • Baba Khalid
  • Riahi Imad (RS Berkane)
  • Salaheddine Errahouli
  • Mouloua Ayoub
  • El Kaabi Youness
  • Lamlioui Oussama (RS Berkane) Morocco wanafungua kampeini Yao dhidi ya Angola siku ya Jumapili Ugani Nyayo kwenye kundi A.
Continue Reading

Trending