Sports
Martin Zubimendi Mali Ya Arsenal

Kilabu ya Arsenal imetangaza rasmi usajili wa kiungo wa Uhispania Martin Zubimendi kwa dau la pauni milioni 51 ambayo inakisiwa kufika pauni milioni 60 badaye.
Mchezaji huyo wa Real Sociadad ametia wino mkataba wa miaka mitano baada ya kupasi vipimo vya kimatibabu ugani Emirates.
The Gunners kwa sasa wako kwenye mazungumzo na mshambulizi wa sporting lisbon victor gyokeres ikiwa sporting wako karibu kukubali dili hiyo kwa pauni milioni 67.
Zubimendi ni mshindi huyo wa kombe la Euro na Uhispania amechezea kilabu yake mechi 236 na taifa lake mechi 19 .
Sports
Harambee Stars Kundi La Kifo Kundi B.

Sports
Kiungo Wa Brenford Bryan Mbeumo Sasa Ni Mali Ya United

Baada ya vute ni kuvute ambayo imedumu kwa kipindi cha mwezi mmoja ni rasmi kwamba kilabu ya manchester United na Brenford wameafikia makubaliano ya pauni milioni 70 ya kiungo mshambulizi Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Haya yanajiri baada ya ofa mara mbili ya united kukataliwa na kilabu hio kabila ya kutuma ofa ya mwisho ya pauni milioni 65 na nyongesa ya pauni milioni 5.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano baada kukubali matakwa yake binafsi.
Mbeumo anakua sajili wa pili kwa kocha mkuu Ruben Amorim baada ya ujio wa mshmabulizi Matheus Cunha.