National News
Mahakama ya Shanzu Yamtaka ODDP Kuwasilisha Mashtaka Mapya Dhidi ya Wakurugenzi Wawili

Mahakama ya Shanzu mjini Mombasa imemtaka Mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma nchini ODPP Renson Ingonga kuwasilisha mashtaka sahihi dhidi ya wakurugenzi wakuu wawili wa chuo kikuu cha North Western Christian waliokamatwa.
Hakimu wa Mahakama hiyo ya Shanzu Leah Juma amepinga mashtaka 120 yaliowasilishwa mbele yake na Ofisi ya mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma dhidi ya washukiwa hao akiwemo Moses Masiga na Jackson Khayumba.
Kulingana na hati kiapo kilichowasilishwa Mahakamani dhidi ya wawili hao, kimeeleza kwamba Masiga na Khayumba wanatuhumiwa kwa kosa la kuendesha chuo ambacho bila kukisajili rasmi kwa Tume ya elimu ya vyuo vikuu nchini.
Katika maelezo zaidi yaliowasilishwa Mahakamani, ni kwamba mnamo Oktoba 13 mwaka 2020 katika mataa wa Bombolulu eneo bunge la Nyali kaunti ya Mombasa wawili hao na wengine ambao hawakuwa mahakamani, walishirikiana kuanzisha chuo hicho bila ya kuzingatia sheria.
Wawili hao pia wanatuhumiwa kutoa vyeti vya kuhitimu kwa mahafali bila ya chuo hicho kusajiliwa, kosa wanalodaiwa kulitekeleza mnamo mwezi Februari 28 mwaka huu katika maeneo ya Nyali kaunti ya Mombasa.
Hata hivyo, wawili hao hawakusomewa mashtaka huku Hakimu mkuu Leah Juma akisema nakala ya mashtaka ilikuwa na kasoro nyingi na kuwaachilia wawaili hao kwa dhamana ya shilingi nusu milioni au pesa taslimu shilingi laki 4 kila mmoja na kesi hiyo ikapangwa kutajwa mnamo tarehe 7 mwezi Aprili mwaka huu.
National News
Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.
Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.
Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.
Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.
National News
Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.
Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.
Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.
Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.
Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.