Connect with us

News

Mahakama ya Kilifi Imeagiza Kuzuiliwa kwa Mshukiwa wa Wizi

Published

on

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa rumande mwanaume mmoja anayekabiliwa na kesi 8 za uvamizi.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike ameagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa hadi tarehe 16 mwezi Mei mwaka huu ambapo uamuzi wa kesi hiyo utatolewa.

Awali kabla ya agizo hilo, Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa anayefahamika kama Victor Otieno, alitekeleza kitendo hicho mnamo tarehe 14 mwezi November mwaka 2024 akiwa amejihami kwa bunduki pamoja na kisu na kumjeruhi Reahma Suley Abdillahi kisha kumuibia simu aina ya Samsug pamoja na runinga yenye thamani ya shilingi laki mbili na elfu ishirini na tisa.

Mahakama hiyo pia imeelezwa kwamba mnamo tarehe 27 November mwaka 2024, mshukiwa akiwa maeneo ya Bofa mjini Kilifi aliweza kuiba simu mbili pamoja na tarakilishi tatu mali iliyomilikiwa na Mzigo Abdallah Juma.

Tarehe 26 Machi mwaka huu katika maeneo ya Kilifi, Victor Otieno alitiwa nguvuni na maafisa wa polisi baada ya kupatikana na pingu na kujifanya yeye ni Afisa wa polisi.

Mshukiwa huyo pia anakabiliwa na kesi zengine 5 tarehe tofauti katika Mahakama ya Kkilifi zinazohushisha wizi wa kimabavu pamoja na umiliki wa bunduki aina ya bastola kinyume cha sharia.

Mahakama hiyo pia imeeleza kwamba mshukiwa anakabiliwa na kesi 16 za uvamizi katika Mahakana ya Malindi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending