Connect with us

News

Mahakama Yaagiza Washukiwa wa Ubakaji Kuzuiliwa Rumande

Published

on

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa rumande washukiwa wawili wa kesi ya ubakaji wa msichana wa umri wa miaka 16, kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa ameagiza washukiwa wa kesi hiyo akiwemo Gift Kalu na Emmanuel Mganga kuendelea kuzuiliwa rumande hadi tarehe 7 mwezi Mei mwaka huu ambapo kesi hiyo itatajwa tena.

Awali kabla ya agizo hilo, Mahakama ameelezwa kwamba washukiwa hao walitekeleza kitendo hicho mnamo tarehe 9 mwezi Aprili mwaka huu katika kijiji cha Mwembetsungu katika kaunti ya Kilifi.

Mahakama pia imeelezwa kwamba wawili hao walitekeleza unyama huo baada ya kumshika shingo na mdomo msichana huyo na kisha kumsukuma kichakani alipokuwa ametoka kuanua viatu nje ya nyumba.

Kesi hiyo itatajwa tarehe 7 mwezi Mei mwaka huu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kindiki, ataka makubaliano kati ya serikali kuu na kaunti kutekelezwa

Published

on

By

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki ametaka makubaliano yote kati ya serikali za kaunti na ile ya kitaifa kutekelezwa kabla ya mwezi Disemba mwaka huu wa 2025.

Akizungumza katika makao yake ya Karen jijini Nairobi Jumatatu 23, Juni 2025, kwenye mkutano wa 27 kati ya serikali kuu na zile za kaunti kuhusu bajeti IBEC, Kindiki alisema kumekuwa na makubaliano ambayo yamekuwa hayafuatiliwi ili kutekelezwa.

Kindiki alisema serikali kuu imejitolea kuhakikisha serikali za kaunti zinafanikisha miradi mbalimbali na kuwataka maafisa wa serikali za kaunti na ile ya kitaifa kushirikiana kwa majadiliano.

Wakati huo huo alisisitiza haja ya kutafuta suluhu la matatizo yanayoathiri utendakazi wa serikali za kaunti huku akipuzilia mbali uwepo wa mzozo wowote baina ya serikali kuu na zile za kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi.

Continue Reading

News

Spika Teddy, adai wabunge wa kitaifa wanachangia kutimuliwa kwake ofisini

Published

on

By

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire ameibua madai kwamba baadhi ya wabunge wa kitaifa kutoka kaunti ya Kilifi ndio ambao wanaendeleza njama ya kumuondoa kama spika wa bunge hilo.

Kupitia video ambayo imekuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, Spika Mwambire alisema viongozi hao wameshirikiana na baadhi ya Wawakilishi wa wadi wa bunge la kaunti ya Kilifi ili kuhakikisha wanafanikiwa kumbandua mamlakani.

Mwambire alisema viongozi pamoja na gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Maitha Mung’aro wako na njama fiche ili kuhakikisha wanatimiza malengo yao ilhali hakuna sababu zozote za kimsingi.

Aidha, Mwambire alisema hadi kufikia sasa hajajua sababu kuu ambazo zinasababisha kutaka kumbandua kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.

Vilevile, alisema hatajiuzulu kama spika wa bunge la kaunti ya Kilifi na kuwakosoa wanaomtaka kuomba msamaha bila kumfahamisha makosa yake.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending