News
Polisi wawili wafariki kwa kupigwa shoti ya umeme

Maafisa wawili wa polisi wamefariki baada ya kunaswa na umema kwenye kituo cha polisi cha Ainamoi eneo bunge la Ainamoi kaunti ya Kericho wakati walipokuwa wakijaribu kuweka nguzo ya mawimbi ya redio katika kituo hicho.
Tukio hilo lilitokea wakati maafisa hao wawili—mmoja wa idara ya upelelezi wa makosa ya jinai (DCI) na mwingine wa jeshi la polisi—waliposhindwa na uzito wa mlingoti, ambao ulianguka na kugusana na nyaya za umeme za moja kwa moja kutoka kwenye njia ya umeme iliyokuwa karibu.
Kulingana na afisa wa utawala wa eneo hilo, kisa hicho kilitokea bila kutarajiwa, na maafisa wote wawili walikufa papo hapo kutokana na shoti ya umeme.
Msamaria mwema aliyekuwa akiwasaidia maafisa hao alipata majeraha madogo baada ya kuangushwa chini na mshtuko mdogo.
Kwa sasa amelazwa katika kituo cha afya cha Ainamoi na inasemekana hali yake inaendelea vyema.
Miili ya maafisa hao wawili ilitolewa katika eneo la tukio na inakisiwa kuwa ilipelekwa katika makafani ya Lazaro katika Hospitali ya Siloam mjini Kericho.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.
Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.
Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.
Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu