Sports
Ligi Limetuponyoka Asema Zico

Mkufunzi wa Kilabu ya Gor Mahia Zedekiah Zico Otieno amekubali kwamba ligi imewaponyoka baada ya kutoka sare na kilabu ya Afc Leopards ugani raila odinga katika debi la Mashemeji jana jioni.
Kiungo matata Austine Odhiambo aliweka uongozini Kogalo kipindi cha kwanza dakika ya 30 kabila ya Brian wanyama kuisawazishia chui dakika ya 55 kipindi cha pili na kocha huyo anaamini taji limewatoka baada ya sare hiyo inayowacha nafasi ya tatu.
“Tulianza Vizuri lakini concetration lapse imetucost kipindi cha pili,lengo letu lilikua kupata ushindi hapa ili kuweka pressure kwa viongozi lakini sasa matokeo haya ni ishara tosha sasa itabidi tuangazie taji la Mozzartbet Cup.”
Kwa upande wake Mkufunzi wa Afc Leopards Fred Ambani amesema kwamba ameridhishwa na matokeo hayo akijigamba angali kupoteza mechi ya Debi akiwa mchezaji na sasa kama kocha wa Ingwe.
“Vijana walioanza mechi kwa mchecheto na uoga mwingi katika kipindi cha kwanza ila tulipoenda katia dressing room nikawambia watulie na ndiposa tukarejea mchezoni,ningali kupoteza debi kama mchezaji sikuwahi na sasa kama kocha pia bado sijapoteza.
Gor inasalia ya tatu na alama 55 huku Afc Leopards wakibaki ya sita na alama 47.
Sports
Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.
Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.
Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.
Sports
Winga Wa Colombia Luis Diaz Sasa Ni Mali Ya Bayern

Klabu ya Bayern Munich, inayoshiriki Ligi Kuu ya Bundesliga nchini Ujerumani, imetangaza kumsajili winga wa Colombia, Luis Díaz.
Hatua hii imekuja baada ya Bayern Munich na Liverpool kufikia makubaliano kuhusu uhamisho wa mchezaji huyo kwa ada ya pauni milioni 65.5.
Díaz, mwenye umri wa miaka 28, aliwasili mjini Munich hapo jana kwa ajili ya vipimo vya kitabibu kabla ya kutia saini mkataba wa miaka minne na mabingwa hao wa Ujerumani.
Mchezaji huyo alijiunga na Liverpool mwaka 2022 akitokea klabu ya Porto kwa ada ya pauni milioni 37. Tangu wakati huo, ameifungia Liverpool mabao 41 katika mechi 142 alizocheza uwanjani Anfield.
Nyota huyo aliondoka kwenye kambi ya mazoezi ya Liverpool mjini Hong Kong hapo jana na kujiunga rasmi na waajiri wake wapya kwa maandalizi ya msimu mpya.