Sports
Ligi Kuu Uingereza EPL Kufungua Milango Yake Hii Leo

Huku Ligi Kuu Uingereza ikifungua Milango rasmi hii leo usiku kilabu ya Arsenal watakabiliwa na mtihani wa mapema wa kuonyesha uwezo wao wa kupigania taji dhidi ya Manchester United iliyofanyiwa maboresho siku ya jumapili jioni, huku mabingwa watetezi Liverpool ikizindua uhasama wa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Uingereza nyumbani dhidi ya Bournemouth saa nne usiku.
Newcastle wanatarajiwa kumkosa mshambuliaji wao nyota Alexander Isak, ambaye anataka kuondoka, katika safari ngumu ya ugenini dhidi ya Aston Villa.
Kama Kipenga Cha Coco FM hebu tuangalie kwa undani jinsi timu zimejipanga kuelekea msimu mpya;
Sajili wapya Benjamin Sseko na Victor Gyokeres;Ni washambulizi wawili ambao wengi watakua wanamulika kwa macho ya ndaani kuona jinsi wataongoza safu zao tofauti za mashambulizi,Wawili hao wanatarajiwa kuanza katika timu zao ugani Old Trafford Jumapili hii.
Kilabu ya Arsenal walimumezea mate mshambulizi Sseko akiwa na RB Leipzig kwa zaidi ya mwaka mmoja kabila badaye kumsajili mshambulizi Victor Gyokeres kwa pauni milioni 64.9 kutoka Sporting Lisbon nyota ambaye pia alikua chaguo la kocha Ruben Amorim wa United kwani waliwahi kufanya kazi pamoja.
Vijana wa Mikel Arteta wakiwa wamemaliza misimu mitatu mfululizo bila kushinda taji la EPL wakisaka mfungaji wa kuwasaidia kufunga zaidi.Na mtu wa kuwapa matumaini hayo ni Gyokeres ambaye katika miaka 2 Sporting alifanikiwa kufunga magoli 97 katika mechi 102.
United msimu jana walikua timu mbovu wakimaliza nafasi ya 15 ligi ya Uingereza kwa mara ya kwanza chini ya Amorim ila sasa wamefanya mabadiliko ikiwemo kusajili nyota Matheus Cunha na Bryan Mbeumo wote ambao walingaa msimu jana na Wolves na Brenford Mtawalia.
Ligi hiyo inpoanzaa leo macho ni kwa Liverpool ambayo licha ya kuwa mabingwa na kuondokewa na badhi ya nyota ikiwemo Alexander Trent Arnold,Luis Diaz na Darwin Nunez wameimarisha kikosi chao kupitia kiungo Florian Wirtz kwa pauni milioni 116,beki Jeremie Frimpong na mshambulizi Hugo Ekitite wakivunja rekodi ya matumizi hadi pauni milioni 260 kwa msimu mmoja.
Wakati vilabu vikuu sita na za jadi Ligi Kuu ya Uingereza—Liverpool, Manchester City, Manchester United, Arsenal, Chelsea na Tottenham—zinavyoendelea kutumia nguvu zao za kifedha kwenye soko la usajili, Aston Villa na Newcastle zimejikuta zikisukumwa pembeni.
Kwa kuwa na vizuizi vya kanuni za uendelevu wa kifedha, usajili mkubwa pekee wa Villa umekuwa ni mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Evann Guessand, aliyejiunga kutoka Nice.
Kocha wa Newcastle, Eddie Howe, amekuwa akipokea maswali ya mara kwa mara kuhusu hali ya Alexander Isak, ambaye alisusia maandalizi ya msimu mpya akilazimisha uhamisho anaoutamani kwenda Liverpool.
Juhudi za The Magpies kumpata mbadala wa mshambuliaji huyo wa Kiswidi zimegonga mwamba mara kwa mara, huku wachezaji kama Sesko, Mbuemo, Hugo Ekitike, Liam Delap na Joao Pedro wakiamua kujiunga na timu nyingine.
Hata hivyo, katika misimu ya hivi karibuni, Villa na Newcastle wamekuwa wakifanya vizuri zaidi kuliko baadhi ya klabu sita kubwa na msimu huu pia wamelenga kufuzu tena kwa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ijumaa;
Liverpool v Bournemouth 22:00pm
Jumamosi;
Aston Villa v Newcastle (5:30pm), Brighton v Fulham, Sunderland v West Ham, Tottenham v Burnley, Wolves v Man City (7:30pm)
Jumapili;
Chelsea v Crystal Palace, Nottingham Forest v Brentford (4:00pm), Man Utd v Arsenal (6:30pm)
Sports
Shirika la Kupiga Vita Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) Lawashtaki Kenya kwa Kukosa Kutii Kanuni

Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za Kusisimua Misuli Duniani (WADA) siku ya Alhamisi limeshtaki Kenya kwa kutotii masharti yake, hatua inayoweza kusababisha nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwekewa vikwazo mwezi ujao.
WADA, lenye makao yake Montreal, Canada, limesema kuwa shirika la kitaifa la kudhibiti matumizi ya dawa za kusisimua misuli nchini Kenya bado halijashughulikia mahitaji muhimu yaliyoainishwa baada ya ukaguzi uliofanywa mwezi Mei 2024.
Kwa sasa, Kenya ina siku 21 za kupinga madai hayo au kufanya marekebisho yanayohitajika na WADA, la sivyo itatangazwa rasmi kuwa imekosa kutii kanuni.
Kwa sasa, kuna wadau wanne waliotia saini kanuni za WADA walioko kwenye orodha ya kutotii masharti. Hawa ni pamoja na:
-
Urusi
-
Sri Lanka
-
Shirikisho la Kimataifa la Basque Pelota
-
Shirikisho la Kimataifa la Mazoezi ya Mwili na Ujenzi wa Misuli (IFBB)
Sports
Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya Ronald Bukusi Afafanua Hali ya Ukocha katika Timu ya Taifa

Mkurugenzi Mkuu wa Cricket Kenya, Ronald Bukusi, ameondoa uvumi kuhusu mpangilio wa uongozi ndani ya timu ya taifa ya kriketi ya wanaume, akisisitiza kuwa hakuna mkanganyiko wowote kuhusu majukumu ya makocha Joseph Angara na Lameck Onyango.
Akizungumza katika makao makuu ya shirikisho hilo Ruaraka, Nairobi, Bukusi alieleza kuwa benchi la kiufundi linafanya kazi kwa mshikamano, huku wachezaji hao wa zamani wa kimataifa wakikamilishana katika uwezo wao.
“Tuna makocha wawili. Inategemea tu wanachofanya siku hiyo maalum,” alisema Bukusi.
Kwa sasa, Angara ndiye kocha mkuu, huku Onyango akiwa msaidizi wake. Wawili hao walichukua majukumu hayo kwa muda tangu Septemba 2024 baada ya bodi kufuta uteuzi wa mchezaji wa zamani wa India, Dodda Ganesh, kwa sababu za ukiukaji wa taratibu.
Kwa kuzingatia kuwa mashindano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la ICC la 2027 yanakaribia, Bukusi alisisitiza kuwa timu ya taifa imedhamiria kazi iliyo mbele yao. Mashindano hayo makubwa duniani yataandaliwa kwa pamoja na Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia.
“Kwa sasa, malengo yetu ni kujaribu kufika Zimbabwe na kufuzu Kombe la Dunia,” alisema Bukusi. “Tuna benchi bora la kiufundi linaloongozwa na Bw. Tariq [mwanabodi], na kwa pamoja tunashughulikia changamoto zinazoikumba timu.”
Hata hivyo, alionya kuwa mafanikio yanahitaji zaidi ya kipaji cha uwanjani, akisisitiza umuhimu wa uwajibikaji na utiifu wa kanuni katika mifumo yote.
“Lazima tuwe watiifu kuhusu fedha na kupiga vita matumizi ya dawa za kusisimua misuli. Sio kitu cha kufanikisha mara moja—itakuwa mchakato,” aliongeza.
Kenya itaendeleza kampeni ya kufuzu kwa kuikabili Namibia Septemba 26 katika Harare Sports Club, kisha kucheza dhidi ya Malawi Septemba 28 katika Takashinga Cricket Club. Mechi yao ya mwisho ya makundi itakuwa dhidi ya Nigeria Septemba 30.
Kenya inatarajia kurudia historia ya mwaka 2003, walipofika nusu fainali, mafanikio makubwa zaidi kuwahi kupatikana na taifa lisilocheza mechi za Test.
-
Entertainment11 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment23 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News20 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni