Connect with us

News

Lagat, kuhojiwa na IPOA kuhusu kifo cha Ojwang

Published

on

Naibu Inspekta jenerali wa Polisi Eluid Lagat, anatarajiwa kufika mbele ya Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi nchini IPOA kuhojiwa siku ya Alhamis Juni, 19.

Lagat ambaye alijiondoa ofisini kwa kuhusishwa na mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang anatarajiwa kuweka wazi anachokifahamu kuhusu mauaji ya Ojwang na kwa nini alitoa idhini ya kukamatwa na kutendewa unyama huo.

Akizungumza na Wanahabari, Mwenyekiti wa Mamlaka ya IPOA Issack Hassan alisema yeyote atakaypatikana na hatia katika kesi hiyo ni lazima atachukuliwa hatua kali za kisheria ili haki kwa muathiriwa ipatikane.

Hassan aliwataka wakenya kuwa na subra wakati maafisa wa upelelezi wa IPOA wanapotekeleza majukumu yao kwani Lagat ameagiza kufika mbele ya Mamlaka hiyo ili kuhojiwa na kuandikia taarifa kuhusiana na mauaji ya Ojwang.

“Tumemuagiza Lagat kufika mbele ya maafisa wetu wa uchunguzi wa IPOA kuhojiwa na kuandikisha taarifa kuhusu kesi ya mauaji ya Ojwang kwa hivyo wakenya wawe na subra na yeyote atakayepatikana na tabia atakabiliwa kisheria”, alisema Hassan.

Wakati huo huo Mahakama iliagiza kwamba Afisa mkuu wa Polisi anayesimamia kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi Samson Talam ataendelea kuzuiliwa kwa siku 14 zaidi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending