Connect with us

News

Lagat, kuhojiwa na IPOA kuhusu kifo cha Ojwang

Published

on

Naibu Inspekta jenerali wa Polisi Eluid Lagat, anatarajiwa kufika mbele ya Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi nchini IPOA kuhojiwa siku ya Alhamis Juni, 19.

Lagat ambaye alijiondoa ofisini kwa kuhusishwa na mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang anatarajiwa kuweka wazi anachokifahamu kuhusu mauaji ya Ojwang na kwa nini alitoa idhini ya kukamatwa na kutendewa unyama huo.

Akizungumza na Wanahabari, Mwenyekiti wa Mamlaka ya IPOA Issack Hassan alisema yeyote atakaypatikana na hatia katika kesi hiyo ni lazima atachukuliwa hatua kali za kisheria ili haki kwa muathiriwa ipatikane.

Hassan aliwataka wakenya kuwa na subra wakati maafisa wa upelelezi wa IPOA wanapotekeleza majukumu yao kwani Lagat ameagiza kufika mbele ya Mamlaka hiyo ili kuhojiwa na kuandikia taarifa kuhusiana na mauaji ya Ojwang.

“Tumemuagiza Lagat kufika mbele ya maafisa wetu wa uchunguzi wa IPOA kuhojiwa na kuandikisha taarifa kuhusu kesi ya mauaji ya Ojwang kwa hivyo wakenya wawe na subra na yeyote atakayepatikana na tabia atakabiliwa kisheria”, alisema Hassan.

Wakati huo huo Mahakama iliagiza kwamba Afisa mkuu wa Polisi anayesimamia kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi Samson Talam ataendelea kuzuiliwa kwa siku 14 zaidi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mradi wa Galana Kulalu kukabili uhaba wa chakula nchini

Published

on

By

Serikali imesema inalenga kufikia ekari 3,200 za kilimo katika mradi wa uzalishaji chakula wa Galana Kulalu ifikapo mwishoni mwa mwaka huu wa 2025.
Waziri wa maji, usafi na kilimo nyunyizi Eric Mugaa alisema tayari ekari 1,060 zimepandwa mahindi kwa kutumia mifumo ya umwagiliaji ya kisasa, mazao ya kwanza yakitarajiwa kuvunwa mwezi Oktoba, huku maandalizi yakuongeza mashamba zaidi yakiendelea.
Akizungumza alipozuru mradi wa Galana Kulalu kutathmini maendeleo ya shughuli za mradi huo, waziri Mugaa pia alisema miundombinu mipya ikiwemo mabwawa ya kuhifadhi maji, mifareji ya kunyunyiza maji, na mitambo ya kusukuma maji imejengwa ilikuwezesha shughuli za unyunyizaji.
Wakati huo huo, waziri huyo alidokeza kuwa ujenzi wa Daraja la Sabaki umefikia hatua ya asilimia 50, akidokezakwamba daraja hilo linatarajiwakukamilika hivi karibuni ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya kilimo na vile vilekusafirisha mazao kutoka Galana Kulalu.
Serikali kupitia Mamlaka ya unyunyizi iliahidi kuendelea kushirikiana na sekta za kibinafsi kuhakikisha mradi huo wa Galana Kulalu unakuwa suluhu ya uhaba wa chakula hapa nchini.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending