Connect with us

Entertainment

Kutoka High Heels Hadi Kuimba Peku Stejini, Nyota Ndogo Afunguka

🎙️ “Sauti yangu ndiyo ya kusikiliza – si viatu vyangu.”
Katika dunia ya burudani ambako muonekano hupewa uzito mkubwa, Nyota Ndogo ameamua kuvunja ukimya. Kupitia video yake ya hivi karibuni, msanii huyo maarufu wa Pwani ameweka wazi sababu ya kuimba bila viatu stejini – na jibu lake linauma, linafundisha na linagusa moyo.

Published

on

Katika dunia ya burudani, wasanii hujikuta wakikumbana na mashabiki wa kila aina – wale wanaopenda sana kazi yao, na pia wale wanaouliza maswali au kukosoa kwa mitazamo yao. Hivi karibuni, muimbaji maarufu wa Pwani ya Kenya, Nyota Ndogo, aliamua kujibu swali ambalo limekuwa likizua mjadala mitandaoni: Kwa nini huimbia stejini bila viatu?

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Nyota Ndogo aliweka video akiwa kwenye onyesho la moja kwa moja, akiimba kwa hisia bila viatu. Video hiyo ilisababisha baadhi ya mashabiki kuuliza au hata kukosoa kuhusu muonekano wake huo, jambo lililomchochea kujibu kwa uwazi wa kipekee.

“Wapenzi wangu, nitakuwa najibu lile linalohitaji kujibiwa tu,” Nyota alianza kwa kusema.

Katika maelezo yake ya wazi na yenye kugusa moyo, Nyota Ndogo alisimulia kuwa alipokuwa msichana mdogo anayeanza muziki, alikuwa akivaa viatu vya michuchumio mirefu (high heels) ili aonekane mrefu. Wanaomfahamu vizuri wanajua kuwa urefu wake si mkubwa, na mara nyingi wale wanaomuona kwa mara ya kwanza hushangaa kumwona mfupi kuliko walivyodhani.

Kwa mujibu wake, viatu hivyo virefu viliathiri afya yake ya miguu kwa kiasi kikubwa:

“Miguu yangu ni mikubwa, nilirithi kwa mama. Lakini vile viatu vimeniletea madhara makubwa sana. Sasa ukubwani ndio naona madhara yake. Miguu huuma sana, wakati mwingine hata kutembea huwa shida, hasa mguu wa kushoto ambao huuma kama kidonda.”

Kwa sababu hiyo, amekuwa akilazimika kuvaa viatu vya chini au wakati mwingine kutumbuiza bila viatu kabisa, hasa maumivu yanapokuwa makali sana.

Lakini licha ya hayo, msanii huyo amesisitiza jambo moja muhimu:

“Mkiniona bila (viatu) niacheni tu na musikilize sauti yangu.”

Katika onyesho lake la hivi karibuni lililofanyika mgahawa mmoja Kilifi, ambalo lilikuwa acoustic performance, mashabiki waliweza kushuhudia nguvu ya sauti yake na hisia halisi bila kuangalia muonekano wa nje. Na kama alivyoeleza, onyesho hilo lilikuwa la aina yake:

“It was wow,” alisema Nyota.

Hadithi ya Nyota Ndogo si tu kuhusu muziki au uvaaji wa viatu – ni somo la maisha. Ni ukumbusho kuwa kila msanii ana hadithi ya kipekee nyuma ya pazia. Kabla ya kuhukumu kwa nje, ni vyema kuelewa ndani – na kama alivyoomba, tusikilize sauti yake, si kutazama miguu yake.

Je, umewahi kuhukumiwa kwa muonekano wako bila kueleweka undani wako? Hebu nambie kwenye comment section. 👇

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien

Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Published

on

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.

Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!

Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.

Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.

Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.

Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.

Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.

Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.

Continue Reading

Entertainment

#UlijanjarukaVipi! Safari ya Mpishi Nguli, Don Moses: Kutoka Kukosa Karo Hadi Kuwa Head Chef

Published

on

Katika dunia ya leo ambapo changamoto za kiuchumi zimewaacha vijana wengi wakihangaika, simulizi ya Don Moses ni mwanga wa matumaini kwa wengi.

Akiwa mgeni katika kipindi cha Janjaruka 254, kinachorushwa kila siku ya wiki kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, Moses alisimulia safari yake ya ajabu kutoka kwa kijana aliyezuiwa na karo ya shule hadi kuwa mpishi mashuhuri hadi kuwa Head Chef aliyesimamia wapishi waliosomea fani hiyo chuoni.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne, Moses alikuwa ameweka ndoto ya kujiunga na chuo lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti. Mama yake alipata ajali mbaya, hali iliyolazimu familia kuhamishia raslimali kwenye matibabu badala ya karo yake ya chuo.

“Nilijua wazi kuwa singeweza kulazimisha familia ichague kati ya maisha ya mama na elimu yangu. Ilibidi nitafute njia mbadala,” anasema Moses.

Jiko la YouTube: Darasa la Ukombozi

Akiwa hana karo, lakini akiwa na shauku, Moses alianza kujifunza sanaa ya upishi kupitia video za YouTube. Binamu yake, Moses Gambo, ndiye aliyemfungulia mlango wa maarifa kwa kumtambulisha kwenye tutorials mbalimbali mtandaoni.

Ni ujuzi huo wa mtandaoni uliomfungulia milango ya ajira katika hoteli za kifahari, ambapo aliweza kupanda ngazi hadi kuwa mpishi mkuu (Head Chef) — akiongoza wapishi waliopitia vyuo vya kitaaluma. Ni mafanikio ambayo wengi hawakuyatarajia kutoka kwa kijana ambaye hakuingia darasa la kawaida, bali alikaa mbele ya skrini.

“Najua kwenye upishi kuna kupika mashendea ama kupika chakula kibaya ila sijawahi kufeli. Siku zote mimi ni makini na ratio ya viungo. Ndiyo silaha yangu,” anasema kwa kujiamini.

Mwaka wa Mageuzi: 2020

Kama ilivyokuwa kwa wengi, mwaka wa janga la COVID-19 – 2020 – ndiyo ulikuwa mwaka wa mabadiliko makubwa kwa Moses. Akiwa na muda mwingi na motisha mpya, alianza kupika kibiashara, akihudumia watu waliokuwa majumbani.

“Kabula ya hapo, nilikuwa napika kwa kujifurahisha tu. Lakini corona ilinifungua macho. Nikaanza kuona kuwa mapishi ni biashara yenye nguvu,” anasema Moses.

Karo Iliyogeuka Mtaji

Kipindi fulani baadaye, Moses alipata nafasi ya kujiunga na chuo hatimaye. Lakini kwa mshangao wa wengi, alikataa ofa hiyo kwa hiari na kuomba fedha hizo zitumike kupanua biashara yake ya upishi.

“Nitamudu gharama ya chuo siku moja. Kwa sasa, najenga misingi. Muda wa kusoma utafika,” anasema.

đź’ˇ Ushauri kwa Vijana: Anza na Kile Kilicho Mkono Wako

Don Moses sasa ni sauti ya matumaini kwa vijana wengi wanaohisi kuwa elimu ya juu au mtaji mkubwa ndio tiketi pekee ya mafanikio. Anasisitiza umuhimu wa kuanza na huduma, si lazima mtaji.

“Kama huna kazi wala mtaji, toa huduma kwanza. Ukiwa na bidii na ubunifu, malipo yatafuata,” anashauri.

Leo hii, sehemu kubwa ya mapato ya Moses huingia moja kwa moja kwenye ununuzi wa vifaa bora vya upishi, huku akiendeleza ndoto yake ya kuwa mmoja wa wapishi wakubwa zaidi nchini Kenya.

Continue Reading

Trending