News
KUPPET na KNUT washinikiza nyongeza ya mshahara

Chama cha Walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET, kimeionya Tume ya uajiri walimu nchini TSC dhidi ya kuwasilisha pendekezo lipya linalokinzana na mkataba wa makubaliano wa malipo wa CBA wa mwaka wa 2025-2029.
Katibu mkuu wa KUPPET nchini, Akello Misori alisisitiza kwamba kuna haja ya kutathiminiwa upya kwa marupurupu yote ya walimu, akisema ni lazima mkataba huo unaangaliwe.
Akello alisema ili kuwawezesha walimu kutekeleza makujumu yao vyema, ni lazima serikali kupitia Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuangalia upya mkataba uliopo mezani na kuhakikisha matakwa ya walimu yanatekelezwa.
“Hivi karibuni kutatua na mazungumzo na muajiri wetu na sisi tuko na msimamo kwamba ni lazima nyongeza ya mshahara ya asilimia 50 na marupurupu ya walimu wanaofanyakazi katika mazingira magumu ya asilimia 30 pia iangaliwe upya”, alisema Akello.
Hata hivyo katika hafla tofauti, Naibu Mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha walimu nchini KNUT Aggrey Namisi alisema iwapo hakutakuwa na mwafaka wowote kuhusu pendekezo hilo la CBA basi wataitisha mgomo wa kitaifa kuanzia mwezi Agosti.
“Sisi tuko tayari kufanya kazi lakini pia matakwa yetu ni lazima yaangaziwe na tunaiambia TSC kama itaendelea kugairi mambo yetu ya CBA mpya tutaambia walimu waanze mgomo mwezi Agosti na watakaoumia na wanafunzi wa gredi ya 9”, alisema Namisi.

Katibu mkuu wa KNUT Collins Oyoo
KUPPET na KNUT hata hivyo wanalenga kuweka mezani mahitaji mapya ya walimu wakati wa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wakuu wa vyama hivyo huku suala la nyongeza ya mishahara na marupurupu ya asilimia 50 likipewa kipau mbele.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.
Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.
Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.
Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.
Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.
Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.
Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.
Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.
Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Taarifa ya Joseph Jira