Connect with us

News

KRA Yatangaza Ongezeko la Ukusanyaji wa Mapato

Published

on

Licha ya hali ngumu za kiuchumi zinazoendelea kushuhudiwa nchini, Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA imetangaza kuongezeka kwa mapato yaliokusanywa mwaka wa kifedha 2024/2025 ikilinganishwa na mwaka wa kifedha 2023/2024.

KRA inasema kumekuwa na ongezeko la asilimia 6.8 la ukusanyaji wa ushuru katika mwaka wa kifedha 2024/2025.

Hii ni baada ya KRA kukusanya ushuru wa trilioni 2.61 ikilinganishwa na trilioni 2.40 zilizokusanywa mwaka wa kifedha uliopita.

KRA imeeleza pia imepitisha makadirio ya ukusanyaji wake wa ushuru kwani iliweka makadirio ya kukusanya ushuru wa kiasi cha trilioni 2.56 na kuishia kukusanya trilioni 2.61.

Ukusanyaji wa ushuru katika mashirika ya kiserikali pia umekua kwa kiwango kikubwa huku kodi za ndani kwa ndani kwenye biashara zikiendelea kuongezeka kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa KRA.

Katika ubadilishanaji wa sarafu, Mamlaka hiyo ya ukusanyaji ushuru imesema kuwa shilingi ya Kenya dhidi ya dola ya Marekani pia imeimarika ikilinganishwa na hali ilivyokuwa mwaka wa kifedha uliopita.

KRA sasa inaeleza matumaini ya kuongezeka kwa ukusanyaji wa ushuru katika mwaka wa kifedha ulioanza wa 2025/2026.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending