Connect with us

News

KPA yaekeza mashine za kufyonza vumbi bandarini Mombasa.

Published

on

Mamlaka ya bandari nchini KPA imeanza kutumia mashine za kufyonza ukungu maarufu mist blower fogging units katika bandari ya Mombasa, ili kudhibiti vumbi hatari linalotokana na shughuli za upakuaji mizigo kwa wingi kama vile klinka, makaa ya mawe na jipsam.

Mradi huu wa majaribio ni sehemu ya sera ya “Bandari Kijani”, inayolenga kulinda afya ya wafanyakazi bandarini, watumiaji, pamoja na wakaazi wa maeneo jirani.

Mashine hizo zimewekwa katika gati namba 9 na 10, na zinatarajiwa kufanya kazi kwa pamoja na vifaa vingine vinavyolinda mazingira kama vile eco-hoppers, ili kupunguza kuenea kwa chembechembe ndogo za vumbi hewani.

Meneja mkuu wa maendeleo ya miundombinu katika KPA, Mhandisi Mathews Amuti, alisema hatua hii ni sehemu ya juhudi za KPA kuzingatia viwango vya kimataifa katika utunzaji wa mazingira na uendeshaji wa shughuli zake.

Amuti alisema kuwa utendaji wa mashine hizo utafanyiwa tathmini kabla ya kuamua kama teknolojia hiyo itaenezwa katika maeneo mengine ya bandari.

Aidha mhandisi huyo aliongeza kuwa mradi huu ni moja wapo ya juhudi za kuimarisha uendelevu wa shughuli za bandari na kupunguza athari zake kwa mazingira na jamii.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaanzisha upya kesi ya ulaghai wa pesa

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeanzisha upya kesi ya mwanaume mmoja anayekabiliwa na shtaka la ulaghai wa pesa.

Hii ni baada ya Mwanaume huyo kwa jina Samuel Ngonyo, kuachiliwa kwa dhamana hapo awali lakini alikosa kudhuhuria vikao Mahakamani hali iliyopelekea kesi hiyo kuanzishwa upya.

Hakimu mkuu wa Mahakama hiyo Charles Obulutsa aliagiza jamaa huyo kuzuliwa rumande baada ya agizo la kukamatwa kwake kuidhinishwa na Mahakama baada ya jamaa huyo kupuuza vikao vya Mahakama vya awali.

Kabla ya agizo hilo, Mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe tofauti kati ya mwezi Septemba hadi Oktoba mwaka 2021 katika maeneo la Ganze kaunti ya Kilifi kwa kutumia njia ya ulaghai, mshukiwa alichukua pesa taslimu shilingi elfu 50 ya mlalamishi Grace Sidi Katana.

Mahakama ilielezwa zaidi kwamba mshukiwa alitekeleza kitendo hicho baada kumdanganya Mlalamishi kwamba yeye ni Mwandishi na afisa wa kazi za umma hivyo angemsaidia Moses Katana mtoto wa mlalamishi kupata kazi ya serikali.

Kesi hiyo itaendelea mnamo tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending