Connect with us

News

KPA yaekeza mashine za kufyonza vumbi bandarini Mombasa.

Published

on

Mamlaka ya bandari nchini KPA imeanza kutumia mashine za kufyonza ukungu maarufu mist blower fogging units katika bandari ya Mombasa, ili kudhibiti vumbi hatari linalotokana na shughuli za upakuaji mizigo kwa wingi kama vile klinka, makaa ya mawe na jipsam.

Mradi huu wa majaribio ni sehemu ya sera ya “Bandari Kijani”, inayolenga kulinda afya ya wafanyakazi bandarini, watumiaji, pamoja na wakaazi wa maeneo jirani.

Mashine hizo zimewekwa katika gati namba 9 na 10, na zinatarajiwa kufanya kazi kwa pamoja na vifaa vingine vinavyolinda mazingira kama vile eco-hoppers, ili kupunguza kuenea kwa chembechembe ndogo za vumbi hewani.

Meneja mkuu wa maendeleo ya miundombinu katika KPA, Mhandisi Mathews Amuti, alisema hatua hii ni sehemu ya juhudi za KPA kuzingatia viwango vya kimataifa katika utunzaji wa mazingira na uendeshaji wa shughuli zake.

Amuti alisema kuwa utendaji wa mashine hizo utafanyiwa tathmini kabla ya kuamua kama teknolojia hiyo itaenezwa katika maeneo mengine ya bandari.

Aidha mhandisi huyo aliongeza kuwa mradi huu ni moja wapo ya juhudi za kuimarisha uendelevu wa shughuli za bandari na kupunguza athari zake kwa mazingira na jamii.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending